Tuesday, July 17, 2012
chakula cha hisani
Hapa utakubaliaana nami kuwa kulipatiakana pesa ijioni hiyo.....................wajionea mwenyekiti wa Chakula cha Hisani Brother Nasri na mwekehazina wake Sister Zaynab Kalulu wakimfuatilia katibu Brother Amry J atoe hesabu sahihi za minoti iliyohesabawa jioni hiyo.
Chakula cha Hisani
Katibu Brother Amry .J na walimu walezi Mr. Allawi Mikidadi na Nchimbi Khamisi,wakiwa na furaha ya kuona maendeleo mazuri ya shughuli ya chakula cha hisani ikiwa inaendelea.......shughuli ilifanikiwa sana takribani Millioni 3 zilitarajiwa kukusanywa katika jioni hiyo.Hongereni sana MSATEKU.
Chakula cha Hisani
Mwalimu Mlezi Mr.Khamis Yunus Nchimbi kishiliki katika shughuli ya chakula cha Hisani kilichoandaliwa na MSATEKU kwa lengo la kuboresha mfuko wa Mradi wao ambao upo karibuni kukamilika....hapa alikuwa anakaribisha wageni waalikwa na kuhamasisha suala la kutoa...pembeni kushoto ni Katibu wa Jumuiya Brother AMRY .J na kulia ni Amir mstaafu Brother Mussa Majugwe.
shughuli mbalimbali za MSATEKU
Wakati wa IDD ya Mfungo TATU,Jumuiya ilitimiza SUNNAH ya kuchinja hapa baadhi ya wanajumuiya wa kihakikisha tendo hilo linakamilika alieshika kisu ni Brother Kimaro,wakati ni Brother Ridhiwan na Brother Mohamed....pembezoni ni Brother Amur...hongereni sana wanajumuiya.
Maendeleo ya Mradi
Assalam alaykum............!!!!Jumuiya ya MSATEKU inaelekea kukumilisha ndoto zake mbalimbali iliyojiwekea kwa uwezo wa ALLAH....inawezekana hujui kinachoendelea ndani ya Mbeya kwa hivi sasa mwana Jumuiya wetu.....Tayari shughuli za maandalizi ya Jengo kubwa la Mradi linafanyiwa tathmini ya kina,chini ya mafundi wakuu na Mlezi wetu.Imani yangu wataka kujionea picha za huko Mbeya jinsi mambo yanavyoendelea....tunakuahidi juhudi zinaendelea za kuzipata picha.....mara tu zikitufikia....hatutokuwa na choyo za kukurushia katika blog yako pendwa ya MSATEKU.......tunakutakia mapunziko mema na maandalizi mema ya Mfungo wa Ramadhan......Inshallah AMIN.
Subscribe to:
Posts (Atom)