Thursday, August 9, 2012

falsafa ya mwezi tukufu wa Ramadhan


FALSAFA YA MWEZI MTUKUFU WA RAMADHANI
.
Kwa Kuhusiana na mwezi huu mtukufu wa Ramadhani, Mimi ninapenda kuwaambieni baadhi ya mambo yaliyo muhimu kwa sababu sisi ni miongoni mwa wale watu waliobahatika kupata fursa hii kwa mara nyingine tena hata bila ya kumuomba Allah Subhanahu wataala.  Kwa mara nyingi, mwanadamu hawezi kukadiria kiasi cha fadhila alizojaaliwa na Mwenyezi Mungu kwa sababu ya kutokujua umuhimu wake, na vilevile hawezi kushukuru neema hizo wala kufaidika na fursa hizi ambazo amefunguliwa njia zake. Kwa upande mwingine kanuni za fursa nazo ni za aina pekee kama vile ilivyooelezwa katika riwaya mbali mbali kuwa fursa zinakuja kama mawingu na kuondoka vivyohivyo. Fursa hizo hazisubiri wala kumbishia hodi mtu mlangoni mwake mara kwa mara, na hazirejei tena. Wanadamu maishani mwao kwa mara moja au kwa baadhi ya nyakati huwa wanabahatika kupata fursa kama hizo, na kwa hivyo inawabidi wawe wenye kushukuru kwa neema hizo. Na inawabidi kukaribisha neema hizo, na kuzikumbatia na vilevile kushikamana nazo. Kwa hakika kwa lenyewe, maana ya fursa na tawfiq inahitaji pia kuangaliwa. Ama kwa wakati huu, inatubidi sisi tuelewe kwamba mwezi huu mtukufu wa Ramadhani ni miongoni mwa fursa nyingi kubwa ambazo Allah swt. Ametuzawadia.
Kwa hakika hili siyo jambo dogo kuwa maisha yetu kwa kipindi cha mwaka mzima yamepita na tumeweza kuingia kipindi hiki cha mwezi mtukufu wa Ramadhani mwaka huu. Chcochote kile ambacho Qur’ani tukufu imezungumzia kuhusu mwezi huu mtukufu  wa Ramadhani kwetu sisi tunaelewa vyema na taswira ambayo Qur’ani tukufu imetuwekea katika akili na fahamu zetu ni kwamba:
“Shahru Ramadhanalladhii anzala fihil Qur’aan Hudalinaasi wabayinatim minal huda walfurqan.”
Mwezi huu Mtukufu ni mwezi uliyoteremshwa Qur’ani Tukufu kama mwongozo wa wanadamu. (Surat Al-Baqarah; 2:185) Hakika katika Mwezi huu mtukufu Qur’ani Tukufu iliteremshwa kama kuwaongoza wanadamu
 Qur’ani Tukufu inazungumzia kuwa mwezi huu ni wa kuteremshwa Qur’ani tukufu.  Na katika riwaya inapatikana kuwa mwezi huu mtukufu wa Ramadhani unaitwa Rabiul Qulub, yaani ni mwezi wa machipuo kwa ajili ya mioyo. Vile mchipuo unavyokuja ardhini,  ndivo hivyo hivyo mioyo yetu inavyokuwa katika hali ya mchipuo. Ni Kipindi au msimu  wa mchipuko siyo kwa majina tu ya kubadilika kwa kubadilika usiku na mchana.  Kwa hakika wenyewe tunaona na kushuhudia kuwa katika msimu huo hali ya ardhi inakuwa katika sura  tofauti kabisa na misismu mingine.
Katika hali hii tunaona ghafla kwa kudra za Allah Subhanahu Wataala kuwa ardhi ambayo ilikuwa ni ngumu, kavu, tasa, iliyogeuka kuwa  jangwa, ikawa ya mchanga, ilikuwa ya mawe na ambayo haikuwa na maji, sasa inageuka kuwa ardhi laini ambapo tunaona majani na mimea na maua vinachipua.
Katika mmojawapo ya miujiza ni kwamba hakuna mtu ambaye anatifua au kulima  katika ardhi hiyo lakini zile mbegu zilizokuwa zimefukiwa ambazo zilikuwa zimeshakufa tunaona zinapata uhai na kuchipua. Sisi sote tumeona vile majani na mimea inavyochipua kutoka ardhini na inaota na kutoa maua na kutoa mbegu na baada ya hapo tunaona miche na miti hiyo inakauka na huku mbegu zake zinakuwa zimefukiwa kwenye ardhi. Kwa kipindi chote cha mwaka mzima kwa vipindi mbali mbali vya kiangazi kipupwe n.k. mbegu inakuwa imebakia imejificha ndani ya ardhi na inapofika msimu wa kuchipua inajichipua na ndiyo kumaanisha kuwa mbegu hiyo inakuwa imehifadhika katika hali yake ya  kuwa imekufa ndani mwa ardhi.  Kwa hivyo unapowadia wakati wa kuchipua mbegu hiyo ambayo ilikuwa imekufa kwa kipindi chote hicho inaanaza kuota  na kutoa majani na hivyo tunaona ardhi inakuwa kijani.  Kwa amri za Allah Subhanahu Wataala ardhi inageuka kuwa laini. Na hivyo kuwa na uwezo wa kuipokea kwenye udongo wake ile mbegu iliyopo na kuipa uwezo wa kupitia hatua mbalimbali na hadi kufikia kuwa rangi ya kijani kwa kuipatia uhai. Na kwa amri za Allah inapotoa majani inatokezea nje ya ardhi, na hapo inakuwa katika mmea ambao unatoa maua na vilevile kufikia hatua ya kutoa matunda. Kwa hakika mandhari hii inakuwa ni nzuri sana na ya kuvutia!  Matunda yanavyokuwa matamu tunayaelewa na manukato ya matunda hayo yanavyokuwa mazuri tunayaelewa. Kwa kifupi tumeona kuwadia kwa msimu wa mchipuo wa mbegu iliyokuwa imekufa kutokea ardhi ambayo nayo ilikuwa imekufa, sasa inaanza kuchipua na hapo ndio tunaona muujiza mkubwa wa Allah Subhanahu Wataala ukiwa dhahir na bayana mbele ya mwanadamu.
Imeelezwa katika riwaya mbali mbali kuwa mwezi mtukufu wa Ramadhani ni mchipuo wa mioyo na vile vile mchipuo wa Qur’ani tukufu. Hii inamaanisha kwamba moyo ambao tunaodhania kuwa uko katika vifua vyetu sivyo hivyo, si moyo ule ulionyuma ya mapafu,  bali ni moyo ule ambao ni nafsi zetu. Na ambao kwa hakika ndiyo moyo wa hisia wa mwanadamu. Hata hivyo moyo huu wa nafsi, unapitia katika vipindi mbalimbali. Vipindi  vya machipuo, kiangazi, masika nk. Bila shaka wengi tutakuwa tumeshaona vile ardhi inavyoonekana katika kipindi cha baridi, wakati ambapo hewa baridi ipo na unakuta maji yanakuwa yemeganda na barafu inadondoka. Na katika hali hii vitu laini vinaganda na kuwa vigumu na vivyohivyo ndivyo moyo wa mwanadamu unakuwa hivyo. Kuna baadhi ya nyakati katika maisha ya mwanadamu ambapo moyo wake unakuwa umeganda kama vile barafu inavyoganda. Hivyo katika hali hiyo kumkumbuka Allah Subahanahu Wataala kunakuwa ni kugumu sana kwa moyo kama huo. Ndio maana baadhi ya nyoyo zinakuwa zimekufa kama miche na mimea inavyokufa katika nyakati mbalimbali katika mwaka. Na hivyo moyo kama huo haukubali kuongozwa. Ili kutaka moyo huo uwe katika hali nzuri na ya kuweza kuchipua na kuzaa majani na matunda mazuri basi moyo huo wa mwandamu ambao unasemwa kuwa Kalbul-Mu’min ashurihaman, na hivyo ndiyo maana Allah Subhanahu Wataala ameuweka msimu huu wa mwezi mtukufu wa Ramadhani ili nyoyo zetu ziweze kuchipua. Kuja kwa mwezi mtukufu wa Ramadhani pasi na kufanya yoyote mioyo yetu inakuwa laini.  Tumeona siku moja imepita na hata siku ya leo imetupita na hali ya siku iliyopita yaani jana na hali ya siku tuliyopo leo ni tofauti. Ingawaje jua na mwezi vinachomoza na kuzama kama kawaiada na usiku na mchana inakuwa sawa lakini leo tunakuwa na hisia yenye nguvu na ya aina  pekee.  Leo tunakuwa na mtazamo ulio wa kitayari, matayarisho tofauti kabisa na yale tuliyokuwanayo siku iliyopita. Na tunaona kuwa nyoyo zetu zinakuwa tayari kupokea jambo fulani na vilevile zinatafuta jambo fulani.
Nuzul ya Qur’ani tukufu si jambo la kufikiria au kudhania au kama vile tunavyofikiria sisi kwa kawaida. Iwapo kutakuwa na majaaliwa Inshallah tutalizungumzia swala hili kwa mapana zaidi katika nyakati nyinginezo. Kwa hakika sisi tunavyolifikiria suala hili la Nuzul ni kwa kile tunachokiona, yaani kwa kitu chenyewe na kuteremka kwake kidhahiri, kama vile kitu kilichopo juu ya paa la nyumba yetu kikija chini au tone la mvua linalodondoka kutokea mawinguni, ndio hapo  tunaposema kitu fulani kimeteremka yaani kimekuja chini. Sisi tunachukulia kuteremka kama vile kitu kinatoka juu kuja chini kwa mfano kunapokuwa na ile lift katika jengo inapoteremka kutoka juu kuja chini tunasema hiyo imeteremka. Kwa hakika fikra kama hii haiwezekani kuzungumziwa kwa ajili ya Qur’ani tukufu. Qur’ani haijateremka katika sura kama hii tunavyoielewa, yaani katika sura fulani au ilikuwa katika mbingu ya saba sasa ikaja chini kwani mbingu ni juu na ardhi ni chini ndio maana tukasema inateremka, sivyo hivyo. Kwa hakika sivyo hivyo kabisa, kwa hakika Qur’ani tukufu ni nuru, mwongozo na vile vile ni neno la Allah Subhanahu Wataala. Kamwe haikuwa katika sura ya kitu fulani kabla au baada yake. Kama kuna mahala ambapo ni nafasi ya Qur’ani tukufu,  basi si katika sura ya kitu fulani au katika hali fulani na nafasi yake ni katika nyoyo zetu. Moyo wa  mwanadamu ndio nafasi ya Qur’ani tukufu.
Maana ya kuteremka ni kwamba Qur’ani ilikuwa katika hali ambayo mwongozo huu, hidaya hii ya Mola Wetu ilikuwa katika hali ambayo sisi hatuwezi kuifikia. Na ilikuwa ni  nje ya uwezo wa uelewa wetu. Qur’ani  tukufu ilikuwa katika ‘Lawhi Mahafudh’. Lawhi Mahafudh siyo jina la kitu au chombo fulani kama vile tunavyoona fremu za mbao au fremu zilizotengenezwa kwa mawe. Kamwe hatuwezi kusema ni kitu kinachoshikika. Lawhi Mahafudh ni mahala au hadhi. Katika kuumbwa kwa ulimwengu mzima ni mahala pamoja na Qur’ani nafasi yake ndio hiyo ambapo sisi daraja letu ni la chini kabisa kama vile Qur’ani tukufu inavoelezea “
Asfala Safilini.”  (Sura ya 95: Aya 5)
Sasa wakati Qur’ani tukufu ilipokuwa katika hali iliyoifadhiwa kwa hiyo haikuwa wepesi kwetu sisi kuelewa kwani sisi tukiwa katika daraja la Asfala Safilin. Sasa kile ninachowaambieni mimi kuwa Qur’ani haikuwezekana kueleweka, haimaanishi kuwa Qur’ani tukufu ilikuwa ni jambo moja lililogumu kabisa nje ya uwezo wetu, au Qur’ani ilikuwa na maajabu yasiyoeleweka au kulikuwa na matatizo ndani yake, laa, bali Qur’ani daima imekuwa ndio mwongozo wetu na ndio iliyokuwa ikituongoza katika kila jambo na daima imekuwa ikituita sisi katika kutuongoza na daima imekuwa jambo moja lililo wazi  na lililo bayana na lililokuwa limefunguka vizuri kwa kueleweka kwa ukamilifu. Lakini swala lililopo hapa ni kwamba uwezo wa wale waliotaka kuielewa umekuwa na mipaka yake, nafasi zao zimekuwa ni za chini kabisa, uelewa wao pia ni mdogo sana hivyo hawawezi kuielewa Qur’ani tukufu kwa ukamilifu. Kwa mfano, iwapo kutatolewa mhadhara wa kitaaluma fulani wa hali ya juu kwa mtoto mdogo basi itamaanisha kuwa unazungumzia jambo moja lililo na mafumbo mengi taabu na lisilo wazi kueleweka kwa mtoto huyo. Ingawaje wewe unalolizungumzia liko wazi kabisa bayana lakini kwa upande wa pili msikilizaji wako ni mtoto kwani yeye anao upeo mdogo wa kuelewa. Wewe jambo unalolizungumzia ni la hali ya juu kabisa wakati yule anayekusikiliza anao upeo mdogo sana wa kuelewa. Vile vile baadhi ya nyakati inaelezwa kuwa wakati mtu anapozungumza jambo lenye elimu ya hali ya juu basi miongoni mwa wale wasilikilizaji wanasema kuwa jambo unalolizungumzia ni la hali ya juu sana ambalo liko nje ya uwezo wetu wa kuelewa hivyo tunakuomba kidogo urahisishe lugha yako ili watu waweze kukuelewa vyema.
Ndivyo hivyo hivyo ilivyo maana ya Nuzul, yaana kwamba hadi katika hali ya sasa hivi ipo katika hali ambayo inaweza kueleweka vyema kabisa kwa wale wenye upeo mdogo wa kuelewa. Qur’ani tukufu imejaribu kuelezea kila jambo kiasi kwamba kila mtu anaweza kulielewa vyema na kwa hivyo ndio maana inaelezwa kama nuzul (kuteremka).
Kwa hakika Qur’ani imekuwa katika hali ya upeo mkubwa kabisa wa juu wa kueleweka, kama haingekuwa katika hali liyopo ya sasa hivi basi ingelikuwa ngumu sana kuielewa. Na hii ndio maana ya nuzul ya Qur’ani tukufu, yaani kuwepo katika hali ambayo tunaweza kuielewa vyema au tukawa na uwezo au upeo wa kuielewa hiyo. Na pale Qur’ani inapokuwa katika hali ya kuweza kueleweka, basi kwa ulimi wetu tu hatuwezi kuielewa Qur’ani tukufu, au kwa kuisikiliza tu hatuwezi kuielewa Qur’ani tukukufu. Kwa hakika mahala ambapo Allah Subhanahu Wataala ametujalia sisi kuielewa Qur’ani tukufu ni katika kalb yaani moyo wetu. Lakini katika kalb hii, misimu mingi inapitia na mavuno ya aina nyingi yanapitia humo, na sura mbali mbali. Na baadhi ya nyakati moyo huu unakuwa mgumu kabisa kama vile inavyosema pale, “kal Hijara au ashadu kaswatan” baadhi ya nyakati inakuwa kama jiwe, na hata kuzidi ugumu wa jiwe. Baadhi ya nyakati moyo huu unakuwa, “Bal Alahah Kulubu Atfaluha” yaani ikimaanisha baadhi ya nyakati nyoyo zinakuwa kama zimefungwa kwa kufuli, na baadhi ya nyakati moyo wetu unakuwa na machafu au uchafu.
Kwa mujibu wa maelezo ya Qur’ani tukufu, ”Rain ala Kulubihim”, yaani baadhi ya tabaka za uchafu zinakuwa zipo juu ya nyoyo zetu. Nyoyo zao zinakuwa zimefungwa kwa mihuri na Allah Subhanahu Wataala ”Khatamalahu Alakulubihim,” Nyoyo zilizopigwa mihuri. Yaani ni kwamba, baadhi ya mioyo ni mawe, na baadhi ya mioyo ni migumu kuliko hata mawe, baadhi ya mioyo inakuwa imefungwa, na baadhi ya mioyo inakuwa imepigwa mihuri kabisa, na baadhi ya mioyo inakuwa imeishaanza kuwa na uchafu, na baadhi ya mioyo inakuwa na tabaka za maovu mbali mbali. Sasa kwa kutaka nyoyo hizi ziwe zimejihusisha na Qur’ani tukufu, ili kuzileta nyoyo hizi karibu na Qur’ani tukufu, Allah Subhanahu Wataala ndio ametujalia neema hii kubwa ya mwezi huu mtukufu wa Ramadhani. Bila ya sisi kusema, kwa kutambua tu haja zetu, Allah Subhanahu Wataala ametujalia muhula huu. Mwezi huu mtukufu wa Ramadhani ni mwezi wa kuchipua kwa mioyo. Hii inamaanisha kwamba mioyo ambayo ilikwisha kuwa migumu, migumu kuliko hata mawe au mioyo ile ambayo imekwisha fungwa na kupigwa mihuri, basi mioyo yote hiyo katika mwezi  huu mtukufu wa Ramadhani inalainika. Huu ni msimu wa kuchipua na katika kila hali ya ardhi inakuwa laini. Lakini iwapo ardhi hii itawekwa vile ilivyo bila kuzalisha chochote wala kupanda mbegu yoyote au kumwagia maji au kwa kujali basi daima itabakia ardhi iliyokufa kama vile itakavyokuwa imetangulia. Msimu wa kuchipua utakuja na utakwenda lakini ardhi hiyo itabakia ngumu na yenye mawe tupu. Kwa hivyo kuna haja kwetu sisi kuifanya ardhi hii iweze kulainika, inatubidi tuitayarishe tupande mbegu tuimwagilie maji na kupanda kitu chochote katika ardhi hiyo. Ndipo hapo ardhi hiyo itakuwa ina rutuba na yenye kuzaa matunda. Kwa hakika ardhi hii ni ngumu kabisa na kwa  upande mwingine ni msimu wenye maajabu, na msimu wa machipuo, mbegu yoyote utakayoipanda ndani yake itaota yaani itazaa matunda. Na kwa maana hii Allah Subhanahu Wataala ndipo alipouzungumzia mwezi huu mtukufu wa Ramadhani kama ni mwezi wa nuzul ya Qur’ani tukufu.
Kwa hakika swaum ndio mojawapo ya nguzo muhimu ya mwezi huu mtukufu wa Ramadhani. Ukuu na hali ya mwezi mtukufu wa Ramadhani si kwa sababu ya kufunga swaumu, bali utukufu na ukuu wa mwezi mtukufu wa Ramadhani ni kwa kutokana na Qur’ani tukufu. Kwa hakika swaum inakuja katika nguzo mojawapo. Ni utaratibu wa mwezi huu mtukufu wa Ramadhani kwamba tufunge swaum katika mwezi huu.  Na mtu yeyote ambaye hafungi swaum katika mwezi huu mtukufu wa Ramadhani basi mtu huyo hana adabu nzuri. Na vile vile haimaanishi kuwa mtu yeyote anayefunga katika mwezi huu mtukufu wa Ramadhani ataweza kubarikiwa baraka zote za Qur’ani tukufu, au kujipatia baraka zote za mwezi mtukufu wa Ramadhani kwa kufunga swaum moja tu! Kwa hakika swaum inaifanya mioyo yetu kuwa milaini. Na vile vile swaum inatoharisha nafsi zetu kwa uelewa bora wa Qur’ani tukufu na kuweza kukubaliwa Hidaya kwa urahisi.
 Baadhi ya nyakati sisi tunasikia, na vile vile tunatamka senteso hii kwa ndimi zetu wenyewe, na utakuwa umesikia kwa watu wengi, na unapowauliza je kwa nini haukuja katika darsa za masomo ya Qur’ani, darsa za tafsiir na sherehe ya Qur’ani, masomo ya Qur’ani, je kwa nini hakuna darasa ya kutoa masomo ya Qur’ani? Ukasema hivyo, wao watajibu – kwa sababu sisi tunafunga swaum. Kwa hiyo mtu anapokuwa katika hali ya swaum anakuwa hayuko imara sawasawa, yaani anakuwa hana nguvu, dhaifu, hawezi kusimama katika hali ya kuwa na swaum. Sasa unaona vile madhumuni ya swaum yanavyokuwa yameuliwa hapa. Allah Subhanahu Wataala ameifanya Swaumu ili kuweza kuelewa Qur’ani. Kufunga swaum kwetu sisi imekuwa ni kikwazo cha kuelewa Qur’ani. Je kwa nini wewe hauisomi Qur’ani? Je Kwa nini hutimizi wajibu wa ibada zingine? Je kwa nini? Majibu ya maswali haya yote atakwambia kwamba yuko katika hali ya swaum. Je, Swaum inakuwa kikwazo kwa kupata Hidaya? Allah Subhanahu Wataa  Amefaradhisha swaum ili kwamba katika hali ya swaum sisi tuweze kuelewa vyema zaidi na kuwafanya wengineo waelewe vizuri zaidi. Kwa hakika sisi tunavyochukulia kuwa swaum ni kikwazo katika kuielewa Qur’ani kwa hakika ni kisingizio tu.  Kwa hakika hii ni fursa moja ya hali ya juu kabisa na umuhimu wake ni kupita uwezo wa vile tunavyoweza kufikria au kudhania katika akili zetu.
Fursa hii tumepewa na Allah Subhanahu Wataala bila ya sisi kuiomba Kwake, bali hata bila ya kuitaka kwa kupitia njia za kuomba. Kwa hiyo inatubidi sisi tuitayarishe mioyo yetu iwe laini mbele ya Allah Subhanahu Wataala na tuseme, ”Ewe Allah Subhanahu Watalaa mbegu yoyote Wewe unayoipendelea, panda katika mioyo yetu hii iliyo lainika na mimi ninauwakilisha moyo wangu huu laini ukiwa kama ndiyo ardhi laini kwako Wewe.” Na kwa hakika Allah Subhanahu Wataala atapandikiza mbegu ya hidaya katika sura ya Qur’ani tukufu. Kwa hakika ni muhimu sana kuisoma hivyo, na kupata kuielewa kwake vilevile ni muhimu mno kwetu sisi. Na vilevile ni muhimu kwetu sisi kupitisha wakati wetu wa mchana na usiku pamoja na Qur’ani tukufu. Na ni muhimu kwetu kujihusisha na Qur’ani tukufu na vilevile tuwe Waislamu maharam kwa Qur’ani tukufu, maharam ni wale walio halalika na wala tusiwe na-maharam wasiohalalika katika kutokuielewa Qur’ani.
 Yaani tusiwe watu na-maharam kwa Qur’ani tukufu. bali inatubidi tuwe watu maharam  kwa Qur’ani tukufu. Msemo huu wa maharamiati, (uhalalifu ), ni nzuri na unaoeleweka kwa urahisi. Kwa hakika sisi tumezoea kusikia Maharam na na-maharam kwa wanaume na wanawake tu, lakini maharamiati ina wigo mpana zaidi kuliko huu. Wakati unapokwenda kuhiji (Hajj), na wakati unapokuwa umevaa Ihram basi wewe unakuwa mahrimu, basi wewe unakuwa umeingia katika haram ya Allah Subhanahu wataala, na hapo ndipo unakuwa maharam.  Muhurim (yule anayevaa  Ihramu) anakuwa maharim wa Allah Subhanahu Wataala na hapo ndipo anasema, ”labbayk” (nimekuja nimeitikia wito wako), na wakati anaposikia jambo anasema Labbayk. Hapo huyo anakuwa ameingia katika kuta nne, anakuwa ameingia katika haram, na yeye sasa ni Muhirimiaji na hivyo mahrim, na yeye sasa anakuwa ni balozi wa siri za miongozo ya kiroho ya Allah Subhanahu Wataala hivyo ndivyo inavyotubidi sisi tuwe mahrim kwa Qur’ani tukufu. Sisi tusichukulie Qur’ani tukufu kama na-maharam, na wala tusiwe na mwelekeo kama  na-maharam pamoja na Qur’ani tukufu. Tusiishi na Qur’ani kama wageni nayo.
 Kubali Qur’ani tukufu na jambo hili litakuwa ni bora kabisa kwetu kama iwapo tunapata fursa hiyo. Wewe umejionea mwenyewe, kuwa mimea na miche inayoota katika kipindi cha mchipuo na mavuno yake yanayofuatia na hali ya ukijani unaokuwa juu ya ardhi, unabakia kwa kipindi cha mwaka mzima. Hata katika kipindi cha kiangazi baadhi ya ukijani unakuwa bado ukionekana, baadhi ya matunda pia yakiwepo na hata maua pia yanaonekana. Maua haya si maua ya kipindi cha kiangazi, maua haya yanakuwa yanatokana na kipindi kile cha mchipuo ambapo bado yanakuwa yanahifadhika hadi katika kipindi kile cha kiangazi, na hata yanakuwa yanahifadhika katika kipindi cha  baridi. Na maua ya msimu huo wa mchipuo yanakuwa katika msimu mwingine pia. Wale wanaokuwa wamelala katika kipindi cha mchipuo basi vipindi vya misimu mingine inakuwa ni misimu yao pia. Na wale wanaokuwa macho katika kipindi cha mchipuo, basi msimu huo wa mchipuo unakuwa bado uko katika misimu mingine inayofuatia.
Jambo hili liko katika uwezo wetu, na iwapo tutataka sisi kufanya msimu huo na misimu yote ikawa ni misimu ya mchipuo, basi itabidi tuelewe thamani ya mwezi mtukufu wa Ramadhani ili tuweze kufaidika na baraka zake zote katika misimu yote. Tunamuomba Allah Subhanahu Wataala atujalie fursa katika mwezi huu mtukufu wa Ramadhani kwa kutilia maanani thamani na ubora wa kipindi hiki; na Insha’allah kwa uwezo wa Allah Subhanahu Wataala sisi sote tutajitumbukiza katika hidaya ya Qur’ani tukufu.
Wabilahi taaufiki.
 Tamati,
Bil-kheir.


Uteremsho wa Qurani












Adabu za kusoma Qurani























Tuesday, August 7, 2012


Thread: Nike / Puma abuses Allah image on shoes

Overall activity: 0%

Nike Puma shoes with Allah written in Arabic style as logo for shoes have created controversy around the World especially among Muslims. A shoe logo design has been used by Nike Company, which is looked like the name of Allah (GOD). Allah has been written in Arabic style on Nike Puma shoes. Many people have protested Nike for designs and tell them, not to use this design in future. People also said that they will stop using Nike products until or unless they remove the sticker from shoes.
Nike Puma has made one pair of shoes and shoes has contained name Allah at Arabic style and people recognized the name and they have protested Puma a lot. Many people have thrown puma shoes from the store shelves. USA Muslims people are protesting Puma to stop making shoes with this logo.
Many Muslims Brothers have given so many bad comments to Puma for there act. Many people have started promoting there statement to other people to stop using Puma/Nike products. People are boycotting Puma and sending this news to every person of the world and they are telling “Do Not Close Eyes”, see it and boycott Puma. This news has been promoted on forums, twitter, face book, communities and other blogs to boycott Puma.
Protesters are also telling that, people should take out those designs shows immediately at any cost. This can not be bearable. Not only Muslims, Hindus are also protesting Puma to stop selling those designs. You can see Hindu, Muslim comments on puma in face book, communities. Every person are protesting them and telling them to stop making those design.
Many people have written petition for Puma / Nike shoes act. There are many people over the world protested. It is really essential for Puma to stop making those designs, because people are boycotting them again and again.
Logo has been written in Arabic style, so people recognized it lately but when they recognized that it is the name of supreme power Allah (GOD). Then they started boycotting Puma and Nike.
Nike company has used a design for there shoes which almost look alike ‘Allah’ written in may languages mainly an Arabic style for writing Allah (God),supreme power of the whole world. As follower of any religion, it means we have faith in one superpower, so its our duty to make sure that Nike must stop using this design in future, because its a disgrace to Allah (God).Overall activity: 0%








 
 

Saturday, August 4, 2012

Muundelezo wa makala motomoto za Amir wako mstaafu.

                                              

Sifa njema anastahiki Allah (s.w), rehma na amani zimuuendee mbora wa viumbe mtume wetu Muhammad (s.a.w.) na Maswahaba zake na wale wote waliopita katika njia yake hadi siku ya mwisho..AMIN
Ni mwezi wa kufanya biashara na muumba wetu….ameweka mwezi huu kw kuwa Allah anahuruma ya kupitilza kwetu sisi…makala hii inaelezea nyakati muhimu za kujipinda sana katika mwezi huu wa Ramadhwaan:
Nyakati Tatu Muhimu Za Kufanya Ibada – Zisikupite Katika Ramadhaan
Nyakati tatu hizi ni muhimu sana za kufanya ibada kutokana na fadhila zake kuu. Mwenye kupenda kuchuma thawabu nyingi asizikose khaswa katika mwezi huu Mtukufu Wa Ramadhaan ambao ni mwezi wenye malipo maradufu
1-Wakati wa mwanzo: Baina ya Alfajiri na jua kuchomoza:
Usimulizi uliothibiti kutoka katika Swahiyh Muslim (564/1) kwamba Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Maswahaba walikuwa wakibakia macho wakati huo hadi jua kuchomoza kwani ni wakati mja anapogaiwa rizki yake, na ni wakati wenye kheri nyingi, unampa siha nzuri ya mwili binaadamu, na kwa ujumla ni wakati wenye baraka nyingi za kila aina kwani Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliomba:
((اللهم بارك لأمتي في بكورها)) الترمذي, أحمد, أبي داود, ابن ماجه
((Ewe Allaah, wabarikie Ummah wangu nyakati za asubuhi mapema)) [At-Tirmidhiy, Ahmad, Abu Daawuud, Ibn Maajah na imethibitishwa kuwa ni Hadiyth Swahiyh na Shaykh Al-Albaaniy]
Usimulizi huu umetoka kwa Maswahaba kadhaa ambao wameelezea kwamba: "Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alipotaka kupeleka kikosi au jeshi aliwapeleka mwanzo wa asubuhi". Vile vile wamesimulia kwamba: "Swakhar alikuwa mtu tajiri ambaye alikuwa akipelekea biashara zake mwanzo wa asubuhi na matokeo yake ilikuwa ni kufuzu katika biashara na kupata faida kubwa sana".
Wamesimulia Salafus-Swaalih kwamba Ibn 'Abbaas naye alimkataza mtu kulala nyakati hizo alipomwambia:
"قُم، أتنام في الساعة التي تقسَّم فيه الأرزاق؟"
"Inuka! Je, unalala katika saa ambayo rizki inagaiwa?"
Ikiwa basi wakati huo ni kama hivyo ilivyoelezwa juu, basi vipi Muislamu auache wakati huu umpite khaswa katika mwezi huu mtukufu wa Ramdhaan?
Ibnul-Qayyim (Rahimahu-Allaah) katika kitabu chake 'Zaad Al-Ma'aad' amesema: "Usingizi wa asubuhi unanyima rizki kwani huo ni wakati ambao Muumba anaombwa rizki na wakati wa kugaiwa rizki. Hivyo usingizi unanyima rizki isipokuwa kwa dharura. Usingizi wakati huo pia ni madhara kwa mwili…"
Faida nyingine kubwa ya kubakia macho ukimdhukuru Allaah wakati huu:
Si chini ya muda wa saa na nusu utakuwa umepata thawabu za Hajj na ‘Umrah kamilifu:
عن أنس عن النبي صلى الله عليه وسلم ، أنه قال (( من صلى الفجر في جماعة ثم قعد يذكر الله حتى تطلع الشمس ثم صلى ركعتين كانت له كأجر حجة وعمرة تامة تامة تامة) ) أخرج الترمذي صححه الألباني .
Imetoka kwa Anas kwamba Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Atakayeswali Alfajiri katika Jama'ah kisha akakaa anamkumbuka Allaah mpaka likachomoza jua kisha akaswali Raka'ah mbili, atapata ujira kama ujira wa kwenda Hajj na 'Umrah ulio kamili kamili kamili)) [Imetolewa na At-Tirmidhiy na kaisahihisha Al-Albaaniy]
Pindi ukifanya hivyo kwa mwezi mzima utakuwa umechuma thawabu za Hajj na ‘Umrah mwezi mzima. Hizo ni fadhila za siku za kawaida, seuze ukifanya mwezi mtukufu huu wa Ramadhaan? Jitahidi ndugu Muislamu kadiri uwezavyo kuchuma hizi thawabu kubwa ambazo zingelikukalifu mali, tabu za safari na mashaka ya kufika Makkah kutekeleza ibada hizo. Lakini kwa Rahma ya Allaah Ametujaalia tuweze kuzichuma tukiwa majumbani mwetu tena kwa wepesi kabisa. Wanaume thawabu zitazidi ikiwa watatekeleza wakiwa misikitini. Wanawake wanazipata fadhila hizo hata wakiswali majumbani mwao. Hata hivyo, pamoja na ujira wote huu, tusisahau kuwa fadhila hizo hazivunji wala hazifuti fardh ya kwenda Hajj kwa mwenye uwezo, asije mtu akadhani kufanya hayo kutakuwa kumetengua wajiibu wake wa kuhiji au kufanya ‘Umrah.
2- Wakati wa pili: Kabla ya Jua kuzama (Magharibi):
Huu ni wakati ambao bado Muislamu yuko katika Swawm na du'aa yake anayoiomba hairudi:
قال صلى الله عليه وسلم: ((ثلاثة لا ترد دعوتهم: الصائم حتى يفطر والإمام العادل والمظلوم)) وروى الترمذي بسند حسن
Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: (([Watu] watatu du'aa zao hazirudi; mwenye kufunga hadi afuturu/afutari, Kiongozi muadilifu na aliyedhulumiwa)) [At-Tirmidhiy kwa isnaad nzuri]
Kwa hiyo ni fursa ya kuitumia Muislamu aombe du'aa na haja zake wakati huu khaswa pia kwa vile ni wakati ambao Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Amehimiza Atukuzwe kama Anavyosema:
(( وَسَبِّحْ بِحَمْدِ رَبِّكَ قَبْلَ طُلُوعِ الشَّمْسِ وَقَبْلَ الْغُرُوبِ))
((.. na mtakase kwa kumsifu Mola wako Mlezi kabla ya kuchomoza jua na kabla ya kuchwa)) [Qaaf: 39]
((وَسَبِّحْ بِحَمْدِ رَبِّكَ قَبْلَ طُلُوعِ الشَّمْسِ وَقَبْلَ غُرُوبِهَا وَمِنْ آنَاء اللَّيْلِ فَسَبِّحْ وَأَطْرَافَ النَّهَارِ لَعَلَّكَ تَرْضَى))
((…Na umtakase Mola wako Mlezi kwa kumsifu kabla ya kuchomoza jua, na kabla halijachwa, na nyakati za usiku pia umtakase, na ncha za mchana ili upate ya kukuridhisha)) [Twaahaa: 130].
(( وَاسْتَغْفِرْ لِذَنبِكَ وَسَبِّحْ بِحَمْدِ رَبِّكَ بِالْعَشِيِّ وَالْإِبْكَار))
((…Na omba msamaha kwa dhambi zako, na umtakase Mola wako Mlezi kwa kumhimidi jioni na asubuhi)) [Ghaafir: 55]
3- Wakati wa tatu: Suhuur - Kabla ya Alfajiri
Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Amewaaahidi Wacha Mungu Pepo kwa sababu sifa mojawapo yao ni kuomba maghfira kabla ya Alfajiri:
إِنَّ الْمُتَّقِينَ فِي جَنَّاتٍ وَعُيُون)) ((آخِذِينَ مَا آتَاهُمْ رَبُّهُمْ إِنَّهُمْ كَانُوا قَبْلَ ذَلِكَ مُحْسِنِينَ)) ((كَانُوا قَلِيلًا مِّنَ اللَّيْلِ مَا يَهْجَعُونَ)) ((وَبِالْأَسْحَارِ هُمْ يَسْتَغْفِرُون))
((Hakika Wacha Mungu watakuwa katika Mabustani na chemchem)) ((Wanapokea Aliyowapa Mola wao Mlezi. Kwa hakika hao walikuwa kabla ya haya wakifanya mema)) ((Walikuwa wakilala kidogo tu usiku)) ((Na kabla ya Alfajiri wakiomba maghfira)) [Adh-Dhaariyaat: 15-18]
Kisha wamesifiwa tena kwa sifa hiyo hiyo pamoja na nyinginezo:
((الصَّابِرِينَ وَالصَّادِقِينَ وَالْقَانِتِينَ وَالْمُنفِقِينَ وَالْمُسْتَغْفِرِينَ بِالأَسْحَارِ))
((Wanaosubiri, wanaosema kweli, na watiifu, na wanaotoa sadaka, na wanaoomba maghafira kabla ya Alfajiri)) [Al-'Imraan: 17]
Muislamu asiache wakati huo umpite kwani ni wakati muhimu na wenye fadhila na faida kubwa kwa vile Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Huteremka wakati huo kutoka mbingu ya saba na kuweko mbingu ya ardhi kutukidhia haja zetu:
عن أبي هريرة رضي الله عنه أن رسول الله صلى الله عليه وسلم قال: ((ينزل ربنا تبارك وتعالى كل ليلة إلى السماء الدنيا حين يبقى ثلث الليل الآخر فيقول: من يدعوني فأستجيب له؟ من يسألني فأعطيه؟ من يستغفرني فأغفر له )) البخاري و مسلم
Imetoka kwa Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu 'anhu) kwamba Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: (Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Huteremka (kwa namna inavyolingana na utukufu Wake) kila siku katika mbingu ya dunia (mbingu ya kwanza) inapobakia thuluthi ya mwisho ya usiku na Husema: Nani ananiomba Nimtakabalie? Nani ana shida Nimtekelezee? Nani ananiomba maghfirah Nimghufurie?)) [Al-Bukhaariy na Muslim]
Nani miongoni mwetu asiyemhitaji Mola wake kumkidhia haja zake na kumuondeshea shida zake? Nani asiyekuwa na madhambi asiyemhitaji Mola wake kumghufuria? Hivyo usiache wakati huu ukakupita khaswa kwa vile mwezi huu Mtukufu ambao kila jambo ulifanyalo lina fadhila na thawabu marudufu.
Tunamuomba Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Atuwezeshe kudiriki nyakati hizo tatu na nyingine, tuwe katika ibada katika mwezi huu wa Ramadhaan na miezi yote mingineyo na Atujaalie kheri na Baraka nyingi, Atukidhie haja zetu, Atuondoshee shida zetu na Atughufurie madhambi yetu yote. Aamiyn
Abuu khaythamah
Mussa Abdallah

Makala za Amir Mstaafu kwa Wanajumuiya na Waislamu wote.


                                                                     










...........ndugu zangu Wanajumuiya (MSATEKU) natamiza ahadi yangu ya kuwaletea makala yangu niliyowaahidi,karibu msome na mfahidike na yaliyomo inshallah Amin.........(Mussa Majugwe)
Kufanya Biashara Na Allaah Isiyoanguka  Kwa Kusoma Qur-aan
Sifa njema anastahiki Allah (s.w), rehma na amani zimuuendee mbora wa viumbe mtume wetu Muhammad (s.a.w.) na Maswahaba zake na wale wote waliopita katika njia yake hadi siku ya mwisho..AMIN;
Tukiwa tuko katika mwezi wa Ramadhwaan tunaweza tukaisoma Qur’an wakati huo huo tunafanya biashara isio na anguko na Allah……
Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala):
((إِنَّ الَّذِينَ يَتْلُونَ كِتَابَ اللَّهِ وَأَقَامُوا الصَّلَاةَ وَأَنفَقُوا مِمَّا رَزَقْنَاهُمْ سِرًّا وَعَلَانِيَةً يَرْجُونَ تِجَارَةً لَّن تَبُورَ))
(( لِيُوَفِّيَهُمْ أُجُورَهُمْ وَيَزِيدَهُم مِّن فَضْلِهِ إِنَّهُ غَفُورٌ شَكُورٌ))
((Hakika wale wanaosoma Kitabu cha Allaah na wakasimamisha Swalah, na wakatoa kwa siri na kwa dhaahiri katika Tulivyowaruzuku, hao hutaraji biashara isiyododa [isiyoanguka]))
((Ili Yeye Awalipe ujira wao kwa ukamilifu, na Awazidishie kutokana na fadhila Zake. Hakika Yeye ni Mwenye kusamehe Mwenye shukrani)) [Faatwir: 29-30]
Aayah hiyo ya mwanzo inajulikana kwamba ni 'Aaayatul-Qurraa' (Aayah wa wasomaji). Ni Aayah pekee katika Qur-aan inayojulikana hivyo. Anasema Shaykh Abu Bakar Al-Jazaairy katika kuifasiri kwake, kwamba: "Aayah hii inawahusu wale ambao wanaikhitimisha Qur-aan kila mwezi au chini ya mwezi". Na hivyo ndivyo Sunnah ilivyo kuikhitimisha Qur-aan kila mwezi kama ilivyo dalili katika usimulizi kwenye Al-Bukhaariy.
Biashara ya mwanzo ni kusoma Qur-aan. Biashara hii bila ya shaka itakuletea faida kubwa utakapoifanya mwezi huu mtukufu wa Ramadhaan kwa vile ndio mwezi ulioteremshwa Qur-aan:
((شَهْرُ رَمَضَانَ الَّذِيَ أُنزِلَ فِيهِ الْقُرْآنُ هُدًى لِّلنَّاسِ وَبَيِّنَاتٍ مِّنَ الْهُدَى وَالْفُرْقَان))
((Mwezi wa Ramadhaan ambao imeteremshwa humo Qur-aan kuwa ni uongofu kwa watu, na hoja zilizo wazi za uongofu na upambanuzi)) [Al-Baqarah: 185]
Vile vile:
حم ﴿1﴾  وَالْكِتَابِ الْمُبِينِ ﴿2﴾ إِنَّا أَنزَلْنَاهُ فِي لَيْلَةٍ مُّبَارَكَةٍ إِنَّا كُنَّا مُنذِرِينَ ﴿3﴾  فِيهَا يُفْرَقُ كُلُّ أَمْرٍ حَكِيمٍ ﴿4﴾
1.        Haa Miym
2.        Naapa kwa Kitabu kinachobainisha
3.        Hakika Tumekiteremsha katika usiku uliobarikiwa. Hakika Sisi ni Waonyaji.Katika usiku huu hubainishwa kila jambo la hikima
[Ad-Dukhaan: 1-4]
Vile vile
إِنَّا أَنزَلْنَاهُ فِي لَيْلَةِ الْقَدْرِ
1. Hakika Sisi Tumeiteremsha Qur-aan katika Laylatul Qadr, Usiku wa Cheo Kitukufu)) [Al-Qadr: 1-5]
Kwa hiyo mwezi wa Ramadhaan ni mwezi wa Qur-aan na kuisoma kwa wingi ndivyo inavyopasa kwa kila Muislamu.Ikiwa kusoma herufi moja ni sawa na thawabu kumi kama alivyosema Mtume صلى الله عليه وآله وسلم ,
عن عبدالله بن مسعودٍ رضي الله عنه أن النبيَّ صلى الله عليه وسلّم قال: (( من قَرأ حرفاً من كتاب الله فَلَهُ به حَسَنَةٌ، والحسنَةُ بعشْر أمْثالها، لا أقُول الم حرفٌ ولكن ألفٌ حرفٌ ولاَمٌ حرفٌ وميمٌ حرفٌ)) رواه الترمذي.
Imetoka kwa 'Abdillaah bin Mas'uud (Radhiya Allaahu 'anhu) kwamba Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema, ((Atakayesoma herufi moja katika kitabu cha Allaah atapata hasanah (jema) moja, na kila hasanah moja ni sawa na thawabu kumi, wala sisemi 'Alif-Laam-Miym' ni herufi moja, bali Alif ni herufi moja na Laam ni herufi moja na Miym ni herufi moja)) [At-Tirimidhiy]
Utakaposoma tu:
﴿ بِسْمِ اللّهِ الرَّحْمَنِ الرَّحِيمِ ﴾
((Bismillahir-Rahmaanir-Rahiym))
ambayo ina herufi 19 hivyo 19 x 10 ni sawa na thawabu190.
Suratun-Naas (Qul A'uudhu Birabbin-Naas) ina herufi 80. Hivyo 80 x 10 = 800 thawabu ambazo utazichuma kwa chini ya dakika moja! Basi itakuwaje biashara hii utakapoifanya kwa kusoma ukurasa mzima? Au robo juzuu? Au nusu juzuu? Au juzuu nzima n.k.? Je, itakuwaje thawabu endapo utakhitimisha Qur-aan nzima?
Jibriyl alikuwa akiteremka kila Ramadhaan kumsikiliza Mtume صلى الله عليه وآله وسلم akisoma Qur-aan na kumdarisisha:
"كَانَ رَسُولُ اللَّهِ -صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ- أَجْوَدَ النَّاسِ وَكَانَ أَجْوَدُ مَا يَكُونُ فِي رَمَضَانَ حِينَ يَلْقَاهُ جِبْرِيلُ وَكَانَ يَلْقَاهُ فِي كُلِّ لَيْلَةٍ مِنْ رَمَضَانَ فَيُدَارِسُهُ الْقُرْآنَ" رواه البخاري
Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa ni mbora (mwenye matendo mema) wa watu, na alikuwa mbora zaidi katika Ramadhaan kwa sababu Jibriyl alikuwa akimjia kila usiku wa Ramadhaan akimfundisha Qur-aan)) [Al-Bukhaariy]
Hali Za Maswahaba Na Salafus Swaalihiyn (Wema Waliotangulia) Na Qur-aan Katika Ramadhaan:
'Uthmaan bin 'Affaan alikuwa akikhitimisha Qur-an kwa siku moja.
Baadhi ya Salaf walikuwa wakikhitimisha kila siku tatu, wengineo kila wiki, wengineo kila kumi moja. Walikuwa wakiisoma Qur-aan katika Swalah na nje ya Swalah.
Imaam Ash-Shaafi'y alikuwa akikhitimisha Qur-aan mara nyingi mno katika Ramadhaan.
Al-Aswad alikuwa akhitimisha kila siku mbili.
Az-Zuhri alikuwa inapoingia Ramadhaan alijitenga na vikao vyote hata vya elimu na alikuwa akishughulika na kusoma Qur-aan pekee.
Salafus Swaalih aliyekuwa na duka, alikuwa akifunga duka lake mwezi wa Ramadhaan akishughulika kusoma Qur-aan pekee.
Adabu za kusoma Qur-aan:
1.        Kupiga mswaki
2.        Kuchukua wudhuu
3.        Kuelekea Qibla
4.        (Wanawake) kujifunika vizuri
5.        Kuelekea Qiblah
6.        Anza na Isti‘adha na BismiLLaah
7.        Soma kwa sauti ya kupendeza.
8.        Zingatia maneno ya Mola wako kwani ni amri kutoka Kwake:
((كِتَابٌ أَنزَلْنَاهُ إِلَيْكَ مُبَارَكٌ لِّيَدَّبَّرُوا آيَاتِهِ وَلِيَتَذَكَّرَ أُوْلُوا الْأَلْبَابِ))
((Na hiki Kitabu, Tumekuteremshia wewe, kimebarikiwa, ili wazizingatie Aayah zake, na wawaidhike wenye akili)) [Swaad: 29]
1.        Unapopita kwenye Aayah za adhabu jikinge nazo; muombe Allaah Akuepushe na adhabu na moto, na unapopita katika Aayah za Rahma na Pepo usiache kumomba Allaah Akupatie hiyo pepo.
Tunamuomba Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Atubarikie wakati wetu na Atuwezeshe kuifanya biashara hii kwa wingi khaswa katika mwezi huu Mtukufu. Aamiyn.
Abuu khaythamah
Mussa Abdallah