Sunday, November 11, 2012

moja ya mada iliyowasilishwa katika semina elekezi ya mwaka wa kwanza (I)


Bismillahir Rahmanir Rahiim:

Brother Amry Jaribu (Msateku - Head Secretary)

I'M PROUD TO BE A MUSLIM:

1:) Islam is the religion of peace

 2:) Islam is the religion of peace and justice

3:) Islam is the religion of peace and tolerance

4:) Islam is the religion of peace and prosperity.

YOUR BROTHER: Amry Jaribu, Don’t forget me in your nice prayers THANKS.

Jumapili,tarehe 11 Novemba, 2012. Assalam alaykum……

Hatuna budi kumshukuru Allah kwa kutupa nguvu na uzima wa kukutana wote hapa katika msikiti wa jumuiya ya MSATEKU kwa lengo la kuambiana mambo mawili,matatu kuhusiana na maisha ya kuwa MWANAFUNZI WA TEKU NA KUJIANDAA ILI KUFAULU VIZURI.Namuomba Allah awapeni usikivu na mie kunipa nguvu ya kuwasilisha mada yangu kwenu,wanafunzi wa mwaka wa kwanza(I) na wengineo………..awali ya wote na nitaanza mada yangu kwa  chachu hizi….

 

 

NAMNA YA KUFELI SHULE KWA MAKUSUDI

1.Usiwe na ratiba ya kujisomea

2.Usiende maktaba kusoma wala kujikumbusha ulivyo soma darasani kwa muda wako wa ziada.

3.Usisome vitabu, wewe soma tu 'summary' za notes na kamusi ili ujue tu maneno magumu ya kuwatishia wengine kua msomi na lugha ina panda kwa sana.

4.Susia vipindi ukijisikia uvivu lala tu wakati wenzio wako darasani au safiri safari ya mbali kula starehe huko

5.Kesha sana kila siku lala saa tisa usiku au kumi kabisa alfajiri wakati shule unatakiwa kuamka saa moja asubuhi kila siku.

6.Nenda club mara nyingi iwezekanavyo kama vipi kila siku
ukiweza.

7.Kuwa mlevi na mwingi wa wanaume/wanawake wakati uko masomoni.

8.Wakati mwalimu anafundisha wewe piga story na rafiki yako na kubadirishana vi memo chini chini vya kuchekesha au cheza game kwe simu au chochote chenye game.

9.Ukipewa mtihani anza kufanya bila kusoma maelekezo kwanza.

10.Kua mtovu wa nidhani na unaye taka ugomvi kila siku na uende darasani ukiwa umelewa(hili si kwa waislamu).

11.Usisome wakati unategemea kufaulu mtihani kwa miujiza.

12.Usisikilize walimu wako au walezi/wazazi hapa TEKU tutawazungumzia Viongozi wa MSATEKU.

13.Uwe mchelewaji kwenda  kwenye vipindi shule na uwahi kuondoka kwenda nyumbani/bwenini

14.Uwe mpenda sifa,mjuaji wa kila kitu, majivuno ya kwenu mna pesa chuo sio ishu.

15.Mwalimu anapo fundisha usichukue notes kaa tu muangalie kama kideo na ongezea kusinzia ikibidi.

16.Usijali GPA au corse works unayopata baada ya mitihani yako 'after all is just a number!!

17.Waambie wenzio 'wametumwa na kijiji kuja kusoma ndio maana wanajituma sana' na wewe kusoma kwako sio ishu sana, after all chuo kikishindikana unaweza kuwa konda wa magari ya''baba/mama,mjomba,shangazi, baba mdogo nk''

18.Ukipewa maswali ya kujibu usifanye yaangalie tu na hisabati soma kama notes usi kokotoe hata moja 'after all ni ugonjwa wa taifa' na kama mmepewa kazi ya kundi wewe usishiriki chochote endelea na mambo yako upate 'marks' za bure

19.Wakatishe wenzio tamaa ''kufauru masomo sio kufauru maisha'; ' wasomi mbona wengi halafu wote choka mbaya tu (kusoma sio dili) au mkubwa afeli bhana……..

20.Ukiwa hujaelewa darasani usiulize kisa utaonekana mjinga.

What DO`s and DON’T`s  (NINI CHA KUFANYA? KUYAEPUKA HAYA YOTE)
10. Pick your major carefully.(yachukulie mambo yako kwa uangalifu na uzito wake) If your university doesn’t make you declare a major off the bat, don’t. Explore new things. Even if you must declare immediately, remember that you can always change your mind. Quiz people in programs you’re considering. Any regrets?
9. If you need help, ask for it. (kama unahitaji msaada,tafadhali omba)If you don’t understand something, ask your leacturer or leader. Many will help you. Another place to find help is the library, where employees can show you how to format your citations or find articles in academic journals. If you’re ever accused of cheating, your student union can help explain your rights.
8. If you’re going to need an extension, ask early. (kama wahitaji ruhusa omba mapema kabla ya kipindi ua ratiba husika haijafikia)If you ask early enough, many lecturer will grant extensions. But don’t annoy your prof by emailing and asking the night before it’s due.
7. Develop a rapport with your leacturer(kuwa na ukaribu au urafiki na Muhadhili wako). Ask questions, contribute to the discussion, stay after class for a minute to clarify something that you don’t understand. In university, you’ll need to make some effort to get noticed.Lecturer who know and like you may help you find jobs, provide references for grad school and will say yes if you ask them to supervise your independent study.
6. Take care of your mental health.(kuwa makini na afya ya ubongo wako) University is stressful, especially if you’re moving away from home for the first time. If you feel anxious or sad, don’t be ashamed to ask your friends for support. There’s also formal counselling from the school. Eating well and exercising can also help greatly.
5. Pick your roommates for second year carefully. (tafuta rafiki kwa makini kwa mwaka wa pili)Think about how you want to live. Your best friend won’t make the best roommate if he or she has different standards of cleanliness, a weird sleep schedule or a higher tolerance for noise. Talk about things like cleaning and splitting bills before you look for housing together. Read up on the laws before you sign a lease.
4. Get involved.(jichanganye/jishughulishe) If you’re in journalism, write for the school paper. If you’re in fine arts, get your work in student-run shows.  If you’re in business, enter case competitions. Participating in degree-related extracurriculars is a great way to network with future colleagues and learn new things.
3. Don’t bring your laptop to class(usiingie na laptop/ipod darasani). Sure, you can type faster than you can write by hand. But Facebook is pretty tempting when it’s in front of you. Plus, when you type your notes, you’re trying to take down every word, which means you’re not really thinking. The secret to success isn’t to take the most notes, but to take the most thoughtful notes. This is easier achieved on paper.
2. Know how to manage your money.(jua namna ya kuudhibiti pesa zako wako) buying prepared food(magengeni) and getting takeout coffee it will impoverish you also may leads you to debt. so learn to cook. Keep track of your spending for a month, to see where you’re overspending.
1. Learn to manage your time(jifunze kujali muda). This is the most important skill for university. Most of your assignments probably won’t be that difficult, but they’ll take longer than anything you’ve done before. Assignments for different classes will often be due at the same time. If you have several essays due in the last week of the semester, you won’t get them all done unless you start early

ways university is not like high school

1. How you write matters.(namna ya kuandika masuala yako) In high school, your teachers were likely happy if you wrote anything at all, and were probably ecstatic if you wrote something clear and gave an opinion or two. That won’t cut it at university. Leacturer expect essays to be formally structured and to provide analysis backed by evidence. They expect papers to be properly formatted, and they expect you to cite sources according to professional style guidelines. Dashing something off at the last minute — no matter how smart you are — won’t cut it.
2. Class is only a quarter of your course.(darasani ni robo ya kozi yako) New university students often make the false assumption that if they attend most of their classes, they are doing the course. But at university, the sitting in class is only a small part of the work. Most of the course is reading the assigned material, doing research for assignments, preparing presentations, meeting with your prof in her office, and writing essays. You should be doing at least three hours of work outside of class for every hour of class time.
3. No one is checking up on you.(hakuna wa kukufuatilia) Unlike high school, no one will come after you or notify your parents if you are falling behind. In fact, in one way, some lecturers like students who don’t do the work because that leaves them with fewer assignments to grade. So, on day one, scour your course outline and figure out how exactly your grade is going to be calculated. Know when things are due and get them done on time. Keep track of everything you hand in and what your current grade is in every course at every point in the year. Avoid unpleasant surprises at the end of term.
4. Expectations are based on the standards of the discipline. (mafanikio yako yanakutegemea nidhamu yako wewe mwenyewe)Your high school teachers have probably been taught that they need to do whatever they can to make sure you have success, even if it means changing what “success” means.  At university, standards tend to be more rigid. You have done well if you have met the standard that your prof thinks is reasonable for a first-year student in that discipline. Whether you did well relative to your own potential is irrelevant. As far as we’re concerned, your personal potential may not be university material.
5. It’s not about you; it’s about the work you do.(sio suala la wewe umefanya nini ila kazi gani umefanya) Many new university students are used to getting credit for “having really tried hard.” But leacturer aren’t grading you or your effort or your sincerity. They are grading the work you do. Many of your professors will never know your name.  If you are at a large university, they may not recognize you in the hallway.
6.Ongea na watu vizuri ili ufanikiwe
7.Waheshimu wenzako
8.Wajali wenyeji wako na hususani viongozi
9.Ishi ni wenzako vizuri hususani wale wa karibu yako mfano waislamu.
10.Jiheshimu mwenyewe kabla ya kuheshimiwa.


NAMNA YA KUJISOMEA VITABU :

Suala la kujifunza kwa kiasi kikubwa linafungamana na kusoma vitabu, kwa hiyo, tumeonelea tuzungumzie suala la kujisomea vitabu  kwa njia ya ufanisi zaidi.
Kwa bahati mbaya wanafunzi wengi tunajisomea vitabu kama wanavyosoma vitabu vya riwaya(hadithi) au visa. Yaani wanaanza kusoma ukurasa wa kwanza na kuendelea kusoma moja kwa moja hadi ukurasa wa mwisho. Wakati kwa hakika hii si njia nzuri ya kusoma vitabu hususani vitabu vya kiada. Kwani vitabu vya kiada vimeandikwa kwa lengo la kufundisha masomo yaliyomo ndani yake. Na vitabu vya kiada vimegawanywa kwa sura.
Na kila sura imegawanywa katika vitengo, na kila kitengo kina anuani yake. Na hii ni tofauti na vitabu vya riwaya(hadithi) ambavyo vimeandikwa kwa mtiririko mmoja kuanzia
mwanzo hadi mwisho.
Kwa hiyo yapasa kuzingatia kuwa anuani za vitabu vya kiada ni nukta muhimu zinazoonesha kitabu kinafundisha nini na katika ukurasa gani. Kwa hiyo, ni jambo zuri kusoma vitabu vya kiada kwa njia maalum kama walivyoibainisha wataalamu.

Njia tuliyoichagua kwa ufipisho inaitwa (KUSUKH), na kirefu chake ni:
• K ----- Kagua:
• U ----- Uliza:
• S ----- Soma:
• U ----- Uliza:
• K ---- Kariri:
• H ---- Hakiki:

Jinsi ya kuitumia njia ya KUSUKH
1. Kagua: Kabla ya kuanza kusoma, tumia dakika mbili tatu kukagua kile utakachosoma. Hapa tunamaanisha kuwa, soma anuani zote za kifungu utakachokisoma.
Pia hakikisha unasoma muhtasari wa kifungu hicho kama upo. Vilevile soma maswali ya kujikumbusha yaliyoambatanishwa na kifungu hicho kama yapo. Faida ya kufanya hivyo ni kupata fikra ya kile utakachokisoma. Kumbuka faida za kukagua kitu kabla ya kukitumia.
2. Uliza:
Baada ya kukagua, hatua inayofuata ni kuunda maswali ya kukusaidia kusoma kwa ufanisi. Na namna ya kuunda hayo maswali ni kama ifuatavyo: Geuza kila anuani iwe swali. Unaweza kuuliza kwa kutumia maneno yafuatayo: Vipi, lini, wapi, nani, inahusu nini, inafanya nini, muda gain nk. Kwa hakika ukibadilisha anuani na kuzifanya kuwa maswali, hilo linakusaidia kutambua wataka kufanya nini na kwa wakati gani.

3. Soma: Hatua ya tatu unatakiwa usome kwa makini kifungu chote ili upate majibu ya yale maswali uliojiuliza katika hatua ya pili.Hapa tuwe karibu na matumizi ya karamu na karatasi.Ili kuchukua mambo muhimu.

4. Uliza:
Baada ya kusoma, unda maswali mengine yanayohusiana na ufafanuzi uliotolewa katika kifungu. Kwa hakika maswali yanakupa changamoto za kufahamu na kukumbuka kile ulichokisoma.

5. Kariri
: Katika hatua hii, unatakiwa uyarudie yale maswali uliyoyatengeneza pamoja na majibu yake uliyoyapata katika kusoma kifungu husika. Yaani soma maneno yale yale kimoyomoyo au kwa sauti au fanya vitendo vile vile mara kwa mara, rudia rudia.
Ni vizuri kuandika kwa ufupi maswali na majibu ya kifungu husika, kwani imethibitika kuwa kuandika kunasaidia kufanya mtu ashike vizuri zaidi kile alichokisoma au kukisikia. Pia waweza kutumia maandishi hayo kwa kujiandaa na mtihani yakiwa ndio ufupisho.
6. Hakiki: Hatua ya mwisho ni kufanya uhakiki wa kile ulichojifunza kwa njia ya kusoma. soma maandishi kwa kuyachambua na kufafanua mambo mbalimbali yaliyomo. Funika kitabu na karatasi ya majibu, kisha jiulize yale maswali ya kifungu cha pili, na jaribu kujipima je, unaweza kuyajibu? Kama jibu ni ndio hongera, hata hivyo soma tena katika kitabu ili kuhakikisha kweli umejibu sahihi. Kama jibu ni hapana bado una nafasi, rejea kusoma kurasa za majibu yako na kitabu ili kujiimarisha.


VIDOKEZO KATIKA KUTUMIA NJIA YA KUSUKH.
1. Tumia akili katika kuunda maswali, jiulize maswali ya msingi sio mzaha mzaha, uliza maswali, kabla na baada ya kusoma.
2. Uliza maswali ya kifungu chote.
3. Kabla hujaanza kuandika majibu ya maswali uliyojiuliza, hakikisha umeshasoma kifungu chote.
4. Andika kwa kutumia maneno yako, yaani kwa ufahamu wako. Pia fanya vifupisho kwa mtindo utakaouonelea kuwa unakufaa.
5. Usijihangaishe kwa kuandika majibu marefu, bora kuandika maneno mawili matatu yanayokukumbusha tu, kwani wewe hurudii kuandika kitabu!
6. Kumbuka kuwa hayo majibu na ufupisho ni wako, kwa hiyo usihofu kuwa watu wengine hawatoufahamu.

KUSOMA KWA MAKUNDI
What is Group Discussion ?
A group discussion is simply a method instrumental in judging the team spirit, leadership qualities, out of the box thinking, and other managerial qualities in an individual. In a layman’s language, a group discussion is a discussion involving a group of around seven to eight participants.
Do you think an individual can work alone and produce results in an organization ?
The answer is No. Every individual works in a team and has to rely on his fellow workers for his easy working and better output. He has to be a good team player to make his mark in the ever challenging corporate world.

Here are Some Tips for a Successful Group Discussion(namna ya kutengenezakundi la mafanikio katika kusoma)
  • The first and the foremost tip for an individual to perform well in a GD is to learn the art of participation.(jifunze tabia ya kushiriki) Don’t expect others to force you to speak. Take the initiative, participate in the discussion and share your ideas with others. Never shout in a group discussion and always wait for your turn to speak. Remember it’s a discussion, not a fighting ground. Be polite but firm.
  • Try to take the initiative.(kuwa wa mwanzo kuanza kujadili hoja) Don’t wait for the others to start the discussion. Always volunteer yourself and start the discussions in an extremely confident manner. Introduce yourself and your team members and then start with the topic but one thing to remember here is that one must initiate the Group Discussion only when he or she is well versed with the topic. Don’t take the risk if you yourself are not very clear about your thoughts.
  • A leader is the one who actually gives the group discussion a direction and guides other team members when they seem to be lost or confused. Like a true leader, an individual must try his level best to refrain from personal favours. Don’t only ask your acquaintance to speak, give equal opportunity to other participants as well. As the leader of the group, he must ensure that the discussion does not end up in fighting and reaches a conclusion.
  • One must speak only if he is well prepared with the topic. (mtu azungumze kwa kujua nini anazungumza yani awe amejiandaa na mada au kinachojadiliwa)Don’t just speak for the sake of points or marks; speak only when you are absolutely sure about what you are speaking. Never depend on guess works in group discussions as it sometimes can seriously go against you. Avoid using slangs or crack jokes in between the discussions as it is considered highly unprofessional.
  • Never be rigid in group discussions.(usiwe mbishi jitahidi kubadilika) Always keep in mind that the other person is also as learned as you. Always listen to what he is saying and then only respond. Be a good and a patient listener. Don’t just simply draw conclusions as there is always a room for discussions. Debate logically and sensibly and try to take everyone along with you.
  • Read a lot and always keep your eyes and ears open.(kuwa makini na usiwe mtu wa kuuliza maswali hovyo) Always begin your day with the newspaper and know what is happening around you. An individual must be aware of the current events to succeed well in a group discussion.
  • Be alert always.(kuwa makini na unachokijadili na kuwa mwangalifu na tabia yako yaani jitambue) A participant usually gets around 15 minutes to think about the topic. You need to think fast and cover as much as you can. Always take care of your words. The content has to be sensible, crisp and well supported with examples or real life situations. Don’t adopt a laidback attitude or yawn in between group discussions.
  • Take care of your dressing as well.(kuwa makini na muangalifu na mavazi yako) Don’t wear flashy(zinazong`aa) clothes while going for a group discussion or interview. Female candidates should also avoid cakey makeup or flaunt heavy jewellery. The clattering sounds of bangles sometimes act as a disturbing element in formal discussions. Be in professional attire and avoid loud colours.
  • An individual must keep in his mind that group discussion is meant for bringing out the managerial skills of an individual. The organizer of the group discussion will never appreciate you or give you the credit if you shout or fight in group discussions. Be calm, composed, confident and neutral to create an impression in the discussion and win over others.

 

Do's and Dont's in a Group Discussion(Nini cha kufanya na kisifanywe katika kundi la majadiliano)

When you are participating in a group discussion, there are a number of things you will want to avoid. While doing the right things can allow you to become a valuable member of the group, doing the wrong things can cause you to disrupt the discussion, and you may find yourself alienated from the other members.
In this article, I will go over the Do's and Dont's of group discussions. By following these guidelines, you will enjoy being a part of group discussions, and you will contribute to the success of the group.

It is important to avoid putting down the ideas that are presented during the discussion.(epuka kuweka kapuni au kudhalau vitu vinavyojadiliwa ) This is especially important if the group is brainstorming ideas. When you put down ideas that are presented by someone else, you are humiliating them in front of the other members, and you are disrupting the brainstorming process. In addition to this, you can create conflict between you and the person you are ridiculing. Never attack the idea of someone else. It can cause other members to be uneasy about sharing their own ideas, because they may fear being ridiculed.

If you don't agree with a statement or idea that has been presented by other another member, address the issue in a polite manner.(kama hujakubaliana na jambo linajadiliwa liwasilishe kwa nidhamu) Instead of attacking their idea directly, why not come up with a better idea instead? It is also important avoid interrupting other members when they are speaking. This is extremely rude. If you feel the need to interrupt someone while they are speaking, try to interject as politely as you can. In some discussion groups, you may be required to raise your hands after someone has finished making a statement. If someone is interrupted by another person why they are speaking, this could create conflict. It may convey a message that what they are saying is not important.

When you are given a task to carry out, it is important for you to do it.(shiriki kufanya kazi ya kikundi) Remember, the group is a machine, and every part of that machine must work if it is to function properly. The members of the group are the pieces that make up the machine. If you are given a task to perform that must be done before the discussion is held, you will want to make sure it is done properly. If it is not done correctly, it can disrupt the flow of the discussion. It is important for you to offer encouragement to the other members. When you encourage the other members of the group, you will gain their respect, and this will allow them to work harder. Encouragement can build up a group discussion, while discouragement can tear it down.

It is important for you to show respect to all the members of the group, and they should show you respect as well.(jiheshimu na utaheshimiwa)When everyone has a mutual respect for each other, this will stop the conflicts which can completely destroy a discussion. If you are the leader of the group, it is essential for you to make sure the right topic is discussed. It should be something that is important to you and the other members. When this is case, the participants will work hard to make sure important issues are covered. If they are not interested in the topic, it will be hard to get them to focus on it. It is important for leaders to choose relevant topics that will be of interest to those who will be participating.

If you are having a brainstorming phase during the group discussion, do not dismiss any ideas that are presented. Give everyone the time to present ideas that they think can be useful in solving problems. Once the brainstorming session is over, let the group decide which ideas are the best.
Another thing that you will want to avoid doing is avoid getting into arguments with other members.(epuka migogoro) It is not productive, and will cause conflicts to occur. While there is nothing wrong with getting into positive arguments, they should not be allowed to get out of control. Show respect to everyone in the group. If you don't agree with a statement that is made by someone, say it in a tactful way.

NAMNA YA KUTENGENEZA GPA

What is a Grade Point Average (GPA)?


 Your Grade Point Average (GPA) is a measure of how well you are doing in your academic studies. At TEKU the academic grading scale goes from “A” to “D”, with corresponding grade points ranging from the highest “5” to the lowest “2”.  A student’s Grade Point Average, or GPA, is a mathematical calculation that indicates where an average of the grades falls on the scale.

Academic/Career/Developmental Programs
Letter Grade
Numerical Grade
Grade Points
Letter Grade Description
A

100-70
5


Excellent.  First Class Standing.  Superior Performance showing comprehensive, in-depth understanding of subject matter.   Demonstrates initiative and fluency of expression.
B+

69-60
4
Very Good.  Second Class Standing.  Clearly above average performance with knowledge of principles and facts generally complete and with no serious deficiencies.
B
59-50
3
Satisfactory or(Good) , Basic understanding with knowledge of principles and facts at least adequate to communicate intelligently in the discipline.
C
40-49
2
Pass.  Some understanding of principles and facts but with definite deficiencies.
D
39-35
1
Minimal Pass( Fail/Supplemantery),A passing grade indicating marginal performance.  Student not likely to succeed in subsequent courses in the subject.
E
 34-0
0
Unsatisfactory (Fail and Exclude), Knowledge of principles and facts is fragmentary; or student has failed to complete substantive course requirements.

2. What is a term grade point average (TERM GPA)?

Your term GPA is the average of your grades for only one semester.
For example, if a student earns grades of “A-“ in all courses, he or she would
have a TERM GPA of 3.67. A GPA of 3.67 or higher, is regarded as first Class Standing
.

How to calculate GPA:
Total of points over Total of Credits = GPA
Ili kuifanya GPA iwe nzuri,tuwe makini na kufanya vizuri kwa masomo yenye CRDTs kubwa mfano crdt 3 kuliko lile lenye CRDTs ndogo,lakini haina maana tuyapuuze yale yenye CRDTs ndogo,yatuongezea idadi ya points pia.Kwa mfano somo lenye CRDTs 3 ukipata A (yaani Grade 5) utakuwa umepata points 15 kuliko somo lenye CRDTs 2 ungepata A (yaani Grade 5) utakuwa umepata points 10.


Kwahiyo tujitahidi kukazania masomo yenye points nyingi kwa ufaulu mzuri. “So let us maintain our Course works”ili kuepuka madhara ya kuharibu GPA yetu.Kwasababu sheria ya TEKU below GPA 1.8 is reapeting a year and not “a DISCO” that is dis-qualified.
Therefore:
First Class
An overall average of 4.4 or higher
 
Upper Second
An overall average in the range of 3.5 – 4.3
 
Lower Second
An overall average in the range of 2.7 – 3.4
 
Pass degree
An overall average of between 2.0 and 2.6

                                                   Wabillah Taufiq..

Semina elekezi kwa ndugu zetu wa mwaka wa kwanza....

Hatuna budi kumshukuru Allah kwa kutupa nguvu ya kuziendeleza kazi za jumuiya yetu ya MSATEKU.......leo tena (Jumapili,tarehe 11-11-2012)MSATEKU kupitia idara yake ya ELIMU iliwaandalia wanafunzi wenzetu wa mwaka wa kwanza (I) semina elekezi ili kufanya maisha yao mapya kwa Chuo cha Teku yawe rahisi,Tunawapongeza idara ya Elimu kwa Kuwaandalia ndugu zetu semina hiyo....chini ni baadhi ya picha hizo......

 Baadhi ya vijana wa mwaka wa kwanza (I) wakifuatila semina elekezi.

 Baadhi ya viongozi wa MSATEKU wakiongozwa na AMIR(MASATEKU) katika mwenye koti jeusi,kushoto ni Amir wa Idara ya Elimu yaBrother Amur......kutoka kulia ni wajumbe wa idara hiyo.Wakifuatilia kwa umakini kile kilichokuwa kinaulizwa na wajumbe.

Brother S-E-S-E-.....nae alikuwepo na makamu Amir wa kitengo cha fedha,akiwa anafanya mawasiliano ili mambo yasiharibike huku semina ikiwa inaendelea.

Ni sehemu ya MATERIALS yanayopatikana katika maktaba yetu ambayo imeanza kufanya kazi,ambapo wanajumuia wanakaribishwa kuja kujisomea materials mbalimbali,imani ya jumuiya maktaba hii kuwa kubwa na yenye kujitosheleza kwa vitabu na mambo mbalimbali ya kujifunzia.

Amir wa Jumuiya akiwa katika ofisi ya jumuiya akianda shughuli mbalimbali za Jumuiya,mara baada ya semina elekezi kuisha mchana wa leo.......pole Brother.......Allah atakulipa kwa jitihada unazofanya za kuipeleka jumuiya ya MSATEKU mbele,mbele yake ni brother Seseme akiwa anahakikisha taarifa za Blog yetu zinawafikia wanajumuiya.......

maendelao ya jengo la mradi wetu......

Assalam alaykum.......wanajumuiya wenzangu,leo tena tunaendelea kupeana maendeleo ya jengo letu la mradi,ambao ujenzi wake unaendelea kwa kasi ili kukamilisha ujenzi wa jengo hilo....hapa chini nawaletea picha nyingine ya jengo hilo,ili kushuhudia kasi ya ujenzi,picha hizi zimechukuliwa leo tarehe 11-11-2012,ya juu ni asubuhi na ya chini ni mchana.


Utakuwa shahidi mwenyewe maendeleo ya jengo hilo yanavyoendelea kwa kasi....Tumuombe Allah alete wepesi katika haya.



Monday, November 5, 2012

maendeleo ya mradi

Hatuna budi kumshukuru Allah....kwa kutupa punzi zake pia kutupa nguvu za kuendeleza yale yote yanayostahiki kwa mwanaadamu kuumbwa hapa duniani.PIa tunashukuru kwa kuweza sasa kuelekea kutimizandoto za wana MSATEKU kwa kuwa na mradi wao pamoja na  msikiti........picha za chini hatua za majengo hayo yalipofikia kwasasa......TAKBIRR>>>>TAKBIRRR>>>>>>TAKBIRRR.....ama hakika hatunabudi kumshukuru ALLAH.




hilo unaloliona ndio jengo....amabalo lipo katika mchakato wake halisi........baada ya muda si mchache itakuwa si hadithi tena.....ALLAH atatulie wepesi inshallah.......AMIN!!!!!!!!!


ukipita nje huo ndio muonekano wake........

Wenzetu hongera kwa kupata degree....!!!

As.alaykum ndugu wanajumuiya.....karibuni sana wale ambao ni wapya katika kufuatilia Blog yetu pendwa ya MSATEKU......hususani wale mwaka wa kwanza (I) ni blog yenye kuleta umoja na mshikamo kati ya wanajumuiya......kwa taarifa tu....mara baada ya kufungua chuo....shughuli za kawaida za jumuiya ziliendelea pamoja na vikao vyake.Siku ya Jumapili ya Jana tarehe 4-11-2012,kulifanyika kiako cha mwezi cha wanajumuiya wot...lakini kabla ya hapo kuilifanyika shughuli ya pamoja ya kusherehekea Idd-il-Haji,ambapo wanajumuiya waliunguna kwa pamoja kusherekea....kama kawaida MBUZI alidondoaka,na mpunga (Mchele) kuliwa.....picha zake nitawaletea zikiwa tayari....lakini Jumamosi ilikuwa shughuli ya mahafali kwa wanachuo wa TEKU......ebu jionee picha chache za kaka zetu nilizobahatika kuzipata....



  hahahhahhahaha....najua utashangaa....hivi huyu wa kushoto katika picha nae amegradueti au mbwembwe tu.........usijali nilikuwa nawapa kampna kaka zangu.........hongerni sana...........









brother Nasri akiwa na wakufunzi wake katikachuo cha TEKU....pembezoni mbaili yakuwa mkufunzi pia ni mlezi wa Jumuiya yetu...Brother Nchimbi.K.Y


Brother Omary(aliyekuwa katibu wa Jumuiya) akiwa nawahitimu wenzake...ama hakika mahafali ilifana.....Hongereni sana wale wote mliogradueti.....

Sunday, October 7, 2012

MAWAIDHA YA ADABU NA TABIA NJEMA.....



ASSALAM ALAYKUM........
 
Ndugu zangu katika imani leo tunajikumbusha tena na kupeana mawaidha ya adabu na tabia njema,ni imani yangu utafuatilia na kuzingatia,ukiwa na maoni tunaomba uyaandike hapo chini,karibu sana......NI mawaidha tunayoayapata kutoka katika blog mbalimbali za kiislamu ili nasi tupitie na kujua yaliyomo katika mawaidha hayo,yametolewa na..........


Muhammad Faraj Salem Al Saiy

Utangulizi

Mwenyezi Mungu ametufunza adabu za namna nyingi ili ziwe pambo letu Waislam zikitupamba katika matendo yetu, maneno yetu, na pia zikitupamba ndani ya nafsi zetu.
Mapambo ya ndani ya nafsi ni Tabia njema. Na Adabu, ni yale maneno na matendo mema yanayozidhihirisha.

Neno Adabu, asili yake linatokana na neno ‘Maaduba’, na maana yake ni kualikwa chakula au kuitwa. Na neno ‘Adabu’, limetoholewa kutoka katika neno hilo ‘Maaduba’, kwa sababu watu ‘Wanaitwa’ katika kuzifuata tabia njema na katika kuwa na khuluka njema.
Khuluka njema ni msingi madhubuti wa Umma. Ni kuendelea kwa Umma. Ni tumaini la Umma. Ni uhai wa Umma.
Umma ukirudishwa nyuma kwa sababu zozote zile za kilimwengu kisha ukapoteza tabia zake njema na khuluqa zake, si rahisi tena kunyanyuka. Lakini Umma hata ukirudi nyuma namna gani, ikiwa bado umeshikamana na khuluqa njema, basi tumaini la kunyanyuka tena linabaki. Na hii ni kwa sababu Umma wowote ukiacha tabia zake njema na kujifanya kama karagosi kwa kuonyesha kila fani ya kuiga, na jeuri na utovu wa adabu, basi tamaa ya kunyanyuka tena inapotea.
Mshairi alisema:
“Hakika ya umma wowote ule ukitaka kubaki, basi lazima wawe na tabia njema. Tabia njema zao zikitoweka, basi na wao watatoweka.”

Umma wa Kiislamu ni Umma uliolelewa kwa Adabu na Tabia njema tokea Mtume wetu Muhammad (Swalla Llahu alayhi wa sallam) alipoanza kuwalingania watu katika dini hii tukufu.
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) alikuwa akisema:
بُعِثْتُ لأتمِّمَ مَكَارِمَ الأَخْلاَقِ
“Kwa hakika nimeletwa kuja kukamilisha (kufundisha) tabia njema”.

Huyu ni Mtume wetu mtukufu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) ambaye Mola wake alimsifia na kumwambia:
وإنك لعلى خلق عظيم
 “Na bila shaka una tabia njema kabisa”
Al Qalam – 4

Muislamu anatakiwa awe mwenye adabu na mwenye heshima akiwaheshimu wakubwa wake na wadodo wake.
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amesema:
<ليس منا من لم يرحم صغيرنا، ويعرف شرف كبيرنا>
Hayupo pamoja nasi asiyewahurumia wadogo wetu na asiyeijuwa heshima ya wakubwa wetu.
Attirmidhy na Abu Daud

Na katika riwaya nyingine, Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amesema kumuambia Ummu Salamah (Radhiya Llahu anha):
يا أم سلمة ذهب حسن الخلق بخير الدنيا والآخرة
Ewe Ummu Salamah, Tabia njema imechukuwa kheri zote za dunia na akhera.
Attabarani

Muislamu asiyekuwa na adabu anaudhuru Uislamu badala ya kuupa nguvu. Mamilioni ya watu waliingia katika dini hii tukufu kwa kuvutiwa na Adabu na Tabia njema za Masahaba (Radhiya Llahu anhum) waliozifungua nchi zao hizo, pamoja na kuvutiwa na Adabu na Tabia njema za wale waliokuja baada yao.
Mataifa makubwa kama vile Indonesia kwa mfano, mamilioni ya watu wake waliingia katika dini hii kutokana na tabia njema za wafanya biashara wa Kiislam waliokwenda huko. Walikuwa wakiuona uaminifu wao, ukweli wao, ucha Mungu wao. Ilikuwa mara tu unapofika wakati wa Swala, walikuwa wakiwaona namna gani wafanya biashara hao wakiacha kazi zao na kuelekea mwahali maalum kwa ajili ya kufanya Ibada zao.
Imam Malik anasema:
“Umma huu hauwezi kutengenea isipokuwa kwa kufuata mwenendo wa wenzao waliowatangulia”.
Kuwatii wazee wawili
Kuwatii wazee wawili ni miongoni mwa Adabu zilizotiliwa mkazo sana na kusisitizwa katika Qurani na katika mafundisho ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam).
Mwenyezi Mungu ametuamrisha tuwatii na kuwafanyia wema wazee wetu, na akazifanya haki za wazee - baba na mama - kuwa katika daraja la pili baada ya haki Zake Subhaanahu wa Taala. Mwenyezi Mungu amewajaalia wazee kuwa ni sababu ya kuwepo kwetu hapa duniani, na kwa ajili hiyo wakapata tabu sana juu yetu.
Hasa Mama, aliyembeba mwanawe tumboni miezi tisa, akamzaa, kisha akahangaika naye na kutaabika naye, tabu juu ya tabu. Tabu ya kubeba, tabu ya kuzaa, tabu ya kulea, kunyonyesha pamoja na kukesha na kuhangaika naye kila mtoto anapolia au kuugua.
Kwa ajili hiyo Mwenyezi Mungu Ametuamrisha kuwakirimu wazee wetu wawili hao, kuwatumikia kuwainamishia bawa la unyenyekevu, pamoja na kuwaombea dua ili Mwenyezi Mungu awarehemu kama walivyotulea huku wakiturehemu tulipokuwa watoto.
Mwenyezi Mungu Anasema:
وَقَضَى رَبُّكَ أَلاَّ تَعْبُدُواْ إِلاَّ إِيَّاهُ وَبِالْوَالِدَيْنِ إِحْسَانًا إِمَّا يَبْلُغَنَّ عِندَكَ الْكِبَرَ أَحَدُهُمَا أَوْ كِلاَهُمَا فَلاَ تَقُل لَّهُمَآ أُفٍّ وَلاَ تَنْهَرْهُمَا وَقُل لَّهُمَا قَوْلاً كَرِيمًا 23 وَاخْفِضْ لَهُمَا جَنَاحَ الذُّلِّ مِنَ الرَّحْمَةِ وَقُل رَّبِّ ارْحَمْهُمَا كَمَا رَبَّيَانِي صَغِيرًا 24

 “Na Mola wako Mlezi ameamrisha kuwa; Msimuabudu yeyote ila Yeye tu, na wazazi wawili muwatendee wema. Mmoja wao akifikia uzee, naye yuko kwako, au wote wawili, basi usimwambie hata: Ah! Wala usiwakemee. Na sema nao kwa msemo wa hishima.
Na uwainamishie bawa la unyenyekevu kwa kuwaonea huruma. Na useme: Mola wanguMlezi! Warehemu kama walivyo nilea utotoni.”
Al israa- Bani Israil 23-24

Na Anasema:
وَوَصَّيْنَا الْإِنسَانَ بِوَالِدَيْهِ حَمَلَتْهُ أُمُّهُ وَهْنًا عَلَى وَهْنٍ وَفِصَالُهُ فِي عَامَيْنِ أَنِ اشْكُرْ لِي وَلِوَالِدَيْكَ إِلَيَّ الْمَصِيرُ
“Na tumemuusia mtu kwa wazazi wake wawili. Mama yake ameichukua mimba yake kwa udhaifu juu ya udhaifu, na kumwachisha ziwa baada ya miaka miwili. (Tumemuusia):Nishukuru Mimi na wazazi wako. Na kwangu Mimi ndiyo marudio.”
Luqman 14

Mafundisho ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) yanakubaliana na mafundisho ya Qurani.
Alipoulizwa juu ya matendo anayoyapenda zaidi Mwenyezi Mungu kupita yote, Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) alisema:
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) alisema:
"الصلاة على وقتها ثم بر الوالدين ثم الجهاد في سبيل اللّه"
"Swala ndani ya wakati wake, kisha kuwafanyia wema wazee wawili kisha jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu."
Fathi l Bari (Sharhi ya Sahihul Bukhari)

Aliiweka amali hii ya kuwafanyia wema wazee wawili kuwa ni ya pili ikiitangulia hata Jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu.

Na alipokuwa akizitaja amali ovu, akaitaja amali ya kuwaasi wazee wawili kuwa ni ya pili baada kumshirikisha Mwenyezi Mungu. Akasema:
قال رسول الله صلى الله عليه وسلم: (ألا أنبئكم بأكبر الكبائر). قلنا: بلى يا رسول الله، قال: (الإشراك بالله، وعقوق الوالدين - وكان متكئاً فجلس فقال - ألا وقول الزور، وشهادة الزور، ألا وقول الزور، وشهادة الزور). فما زال يقولها، حتى قلت: لا يسكت.
Amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam):
“Nikuambieni ni amali zipi zilizo ovu kupita zote?”
Tukasema:
“Tuambie ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu”
Akasema:
“Kumshirikisha Mwenyezi Mungu na kuwaasi wazee wawili,”
Alikuwa ameegemea, akakaa vizuri, kisha akasema:
“Na kusema uongo, na kutoa ushahidi wa uongo…”
Akawa anayakariri maneno hayo mpaka tukasema (nyoyoni);
“Yareti angenyamaza”
Bukhari na Muslim

Pakitokea mgongano baina ya haki ya Mwenyezi Mungu na haki ya wazee, kwa mfano mzee awe ni mshirikina akimuamrisha mwanawe naye awe kama yeye katika ushirikina huo, au katika kumuasi Mwenyezi Mungu kwa jambo lolote lile, basi hapo haijuzu kumtii mzee, kwa sababu haki ya Mwenyezi Mungu ni kubwa zaidi na tukufu zaidi. Lakini wakati huo huo kuasi au kumshirikisha Mwenyezi Mungu kwao, kusikuzuwie kuwatendea mema na kusikufanye ukawa unawapiga pande.
Mwenyezi Mungu anasema:
وَإِن جَاهَدَاكَ عَلى أَن تُشْرِكَ بِي مَا لَيْسَ لَكَ بِهِ عِلْمٌ فَلَا تُطِعْهُمَا وَصَاحِبْهُمَا فِي الدُّنْيَا مَعْرُوفًا وَاتَّبِعْ سَبِيلَ مَنْ أَنَابَ إِلَيَّ ثُمَّ إِلَيَّ مَرْجِعُكُمْ فَأُنَبِّئُكُم بِمَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ
“Na pindi wakikushikilia kunishirikisha na ambayo huna ilimu nayo, basi usiwat'ii. Lakini kaa nao kwa wema duniani, nawe ishike njia ya anayeelekea kwangu. Kisha marejeo yenu ni kwangu Mimi, na Mimi nitakuambieni mliyokuwa mkiyatenda.”
Luqman -15
Ndugu wa Nasaba ni wale ulohusiana nao, jamaa zako, ikiwa ni katika wanaoweza kukurithi au wasioweza, unaoweza kuoana nao au usioweza, lakini upo uhusiano wa nasaba baina yenu.
Mwenyezi Mungu Ametutahadharisha juu ya hatari ya kuwapiga pande ndugu wa Nasaba Akasema:
أَيُّهَا النَّاسُ اتَّقُواْ رَبَّكُمُ الَّذِي خَلَقَكُم مِّن نَّفْسٍ وَاحِدَةٍ وَخَلَقَ مِنْهَا زَوْجَهَا وَبَثَّ مِنْهُمَا رِجَالاً كَثِيرًا وَنِسَاء وَاتَّقُواْ اللّهَ الَّذِي تَسَاءلُونَ بِهِ وَالأَرْحَامَ إِنَّ اللّهَ كَانَ عَلَيْكُمْ رَقِيبًا
“Enyi watu! Mcheni Mola wenu Mlezi aliyekuumbeni kutokana na nafsi moja, na akamuumba mkewe kutoka nafsi ile ile. Na akaeneza kutokana na wawili hao wanaume na wanawake wengi. Na tahadharini na Mwenyezi Mungu ambaye kwaye mnaombana, na jamaa zenu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kuwaangalieni.”
Annisaa - 1
Hapa Mwenyezi Mungu anatutahadharisha tusije tukamuasi, na pia anatutahadharisha juu ya Jamaa zetu, tusije tukawapiga pande na kuachana nao.
Mwenyezi Mungu pia ametutaka tushikamane na kuendeana nao.
Mwenyezi Mungu anasema:
وَإِذْ أَخَذْنَا مِيثَاقَ بَنِي إِسْرَائِيلَ لاَ تَعْبُدُونَ إِلاَّ اللّهَ وَبِالْوَالِدَيْنِ إِحْسَاناً وَذِي الْقُرْبَى وَالْيَتَامَى وَالْمَسَاكِينِ وَقُولُواْ لِلنَّاسِ حُسْناً وَأَقِيمُواْ الصَّلاَةَ وَآتُواْ الزَّكَاةَ ثُمَّ تَوَلَّيْتُمْ إِلاَّ قَلِيلاً مِّنكُمْ وَأَنتُم مِّعْرِضُونَ
“Na tulipofunga agano na Wana wa Israili: Hamtamuabudu yeyote ila Mwenyezi Mungu; na muwafanyie wema wazazi na jamaa na mayatima na masikini, na semeni na watu kwa wema,na shikeni Swala, na toeni Zaka. Kisha mkageuka isipo kuwa wachache tu katika nyinyi; na nyinyi (pia) mnapuuza.”
Al Baqarah - 83

Na Akasema:
وَأُوْلُواْ الأَرْحَامِ بَعْضُهُمْ أَوْلَى بِبَعْضٍ
“Na ndugu wa nasaba wanastahikiana wenyewe kwa wenyewe”
Al Anfal – 75
Na Akasema:
فَآتِ ذَا الْقُرْبَى حَقَّهُ وَالْمِسْكِينَ وَابْنَ السَّبِيلِ ذَلِكَ خَيْرٌ لِّلَّذِينَ يُرِيدُونَ وَجْهَ اللَّهِ وَأُوْلَئِكَ هُمُ الْمُفْلِحُونَ
“Basi mpe jamaa haki yake na masikini na msafiri (aliyeharibikiwa). Hayo ni bora kwa wale wanaotaka radhi ya Mwenyezi Mungu; na hao ndio watakaofuzu”.
Ar Rum – 38

(Neno ‘Rahim’ maana yake ni ‘undugu wa nasaba’)
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amesema:
“Mwenyezi Mungu amelitoa (au amelitohoa) jina la ‘Rahim’ kutoka katika jina lake ‘Al Rahiym’, kisha akasema:
“Atakayekuunga nitamuunga na atakayekukata nitamkata”.
Na hii inamaanisha kuwa Mwenyezi Mungu atamkata (kwa kutomrehemu) yule atakayeukata uhusiano na jamaa zake, na atawaunga (kwa kuwarehemu) wale watakaouendeleza uhusiano huo.

Mtu anaweza kuona kuwa; katika kutembeleana kwa ajili ya kuunganisha uhusiano na ndugu wa nasaba pesa nyingi zinatumika na wakati mwingi unapotea. Lakini Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) ametufundisha kinyume na hivyo.
Katika hadithi ilisiyomuliwa na Anas bin Malik (Radhiya Llahu anhu), Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amesema:
“Anayependa atandaziwe riziki (aongezewe riziki yake), basi aendeleze uhusiano wake na ndugu zake wa nasaba (jamaa zake alohusiana nao)”.
Bukhari
Na katika Hadith al Qudusiy, Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amesema:
“Mwenyezi Mungu ameiambia Rahim; ‘Je utaridhika iwapo nitamuunga atakayekuunga na nitamkata atakayekukata?”
Rahim ikasema:
“Ndiyo”
Mwenyezi Mungu Akasema:
“Basi hiyo ni haki yako”
Bukhari

Kuuendeleza uhusiano huu kunakuwa kwa kupendana, kunasihiana, kufanyiana wema na uadilifu, kurudishiana haki zilizopotea, kuwasaidia wale wenye shida kati yao, kujua hali zao, kusameheana katika makosa yanayotokea baina yao mara kwa mara, kuombeana dua, na kwa ujumla kujaribu kuwafanyia kila la kheri na kuwaepusha na kila shari kwa uwezo wote.
Iwapo katika ndugu, yupo au wapo wasiopenda kurudisha uhusiano na ndugu kwa sababu ndugu yake au jamaa yake huyo anapindukia mipaka katika kumuasi Mwenyezi Mungu, na baada ya kujaribu kila njia katika kunasihi kwa kutumia njia mbali mbali za hekima kujaribu kumweka sawa ndugu huyo bila mafanikio, basi hapana ubaya kuepukana na mtu au watu wa aina hiyo, wakati huo huo tukiendelea kuwaombea dua, huenda Mwenyezi Mungu akawahidi na kuwaongoza katika haki.
Mwenyezi Mungu anasema:
وَاعْبُدُواْ اللّهَ وَلاَ تُشْرِكُواْ بِهِ شَيْئًا وَبِالْوَالِدَيْنِ إِحْسَانًا وَبِذِي الْقُرْبَى وَالْيَتَامَى وَالْمَسَاكِينِ وَالْجَارِ ذِي الْقُرْبَى وَالْجَارِ الْجُنُبِ وَالصَّاحِبِ بِالجَنبِ وَابْنِ السَّبِيلِ وَمَا مَلَكَتْ أَيْمَانُكُمْ إِنَّ اللّهَ لاَ يُحِبُّ مَن كَانَ مُخْتَالاً فَخُورًا
“Muabuduni Mwenyezi Mungu wala msimshirikishe na chochote. Na wafanyieni wema wazazi wawili na jamaa na mayatima na masikini na jirani wa karibu na jirani wa mbali, na rafiki wa ubavuni na mpita njia, na walio milikiwa na mikono yenu ya kulia. Hakika Mwenyezi Mungu hawapendi wenye kiburi wanao jifakhiri”.
Annisaa – 36
Na katika hadithi iliyotolewa na Bukhari, Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amesema:
“Jibril alikuwa akiendelea kuniusia juu ya Jirani, hata nilidhania atapewa haki ya kunirithi”
Kumfanyia wema jirani, ni kwa kutokumuudhi au kumkera.
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amesema:
“Wallahi si Muislam Wallahi si Muislam”,
Wakamuuliza:
“Nani huyo ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu?”
Akasema:
“Ambaye jirani yake haiepuki shari yake”

Katika wema pia, ni kumfanyia jirani ihsani kiasi cha uwezo wako kwa kumsaidia pale anapohitajia msaada wao, kwa kumjulia hali yake, kumpelekea zawadi, yote hayo kiasi cha uwezo.
Mwenyezi Mungu anasema:

يَسْأَلُونَكَ مَاذَا يُنفِقُونَ قُلْ مَا أَنفَقْتُم مِّنْ خَيْرٍ فَلِلْوَالِدَيْنِ وَالأَقْرَبِينَ وَالْيَتَامَى وَالْمَسَاكِينِ وَابْنِ السَّبِيلِ وَمَا تَفْعَلُواْ مِنْ خَيْرٍ فَإِنَّ اللّهَ بِهِ عَلِيمٌ
“Wanakuuliza watoe nini? Sema: Kheri mnayo itoa ni kwa ajili ya wazazi na jamaa na mayatima na masikini na wasafiri. Na kheri yoyote mnayo ifanya Mwenyezi Mungu anaijua”.
Al Baqarah - 215

Na akasema:

وَإِذَا حَضَرَ الْقِسْمَةَ أُوْلُواْ الْقُرْبَى وَالْيَتَامَى وَالْمَسَاكِينُ فَارْزُقُوهُم مِّنْهُ وَقُولُواْ لَهُمْ قَوْلاً مَّعْرُوفًا
“Na wakati wa kugawanya wakihudhuria jamaa na mayatima na masikini, wapeni katika hayo mali ya urithi, na semeni nao maneno mema”.
An Nisaa - 8

Na akasema:

فَآتِ ذَا الْقُرْبَى حَقَّهُ وَالْمِسْكِينَ وَابْنَ السَّبِيلِ ذَلِكَ خَيْرٌ لِّلَّذِينَ يُرِيدُونَ وَجْهَ اللَّهِ وَأُوْلَئِكَ هُمُ الْمُفْلِحُونَ
“Basi mpe jamaa haki yake, na masikini, na msafiri. Hayo ni kheri kwa watakao radhi ya Mwenyezi Mungu. Na hao ndio wenye kufanikiwa”.
Ar Rum - 38
Na katika hadithi, Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amesema:
“Mwenye kujishughulisha kuwasaidia Vizuka na Masikini ni mfano wa anayepigana Jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu, au mfano wa mwenye kufunga nyakati za mchana na kuswali nyakati za usiku”.
Bukhari
Na katika hadithi nyingine Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amesema:
“Mimi na mwenye kumlea yatima tutakuwa (pamoja) Peponi kama hivi.” Akaashiria kwa kidole cha shahada na cha kati.
Bukhari
Mwenyezi kiburi hupata maradhi mengi yakiwemo kudharau, kusengenya nk. Na hii ni kwa sababu mtu wa aina hii siku zote hujiona kuwa yeye amekamilika, na kwa ajili hiyo huanza kuwatia wenzake kila aina ya ila, wakati ukweli wa mambo ni kwamba yeye ndiye mwenye ila, na kwa ajili hiyo utamuona anajaribu kutafuta ila za wenzake pamoja na makosa yao na kuwaonyesha watu makosa hayo, ili ajionyeshe kuwa yeye amekamilika.
Mtu wa aina hii hupenda kuwadharau wenzake na kuwacheka pale wanapokosea.
Haya yote yameharimishwa. Na Mwenyezi Mungu ametujulisha kuwa mwenye kudharauliwa huenda akawa ni bora kuliko mwenye kudharau, na ujinga wa mwisho ni mtu kumdharau yule aliye bora kuliko yeye.
Mwenyezi Mungu Anasema:
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا يَسْخَرْ قَومٌ مِّن قَوْمٍ عَسَى أَن يَكُونُوا خَيْرًا مِّنْهُمْ وَلَا نِسَاء مِّن نِّسَاء عَسَى أَن يَكُنَّ خَيْرًا مِّنْهُنَّ
“Enyi mlio amini! Wanaume wasiwadharau wanaume wenzao, wala wanawake wasiwadharau wanawake wenzao. Huenda hao wakawa bora kuliko wao.”
Al Hujurat - 11

Na katika jambo baya la dharau ni kule kuwavunjia watu heshima na kuwaita kwa majina ya kejeli.
Mwenyezi Mungu Anasema:
وَلا تَلْمِزُوا أَنفُسَكُمْ وَلا تَنَابَزُوا بِالاَلْقَابِ بِئْسَ الاِسْمُ الْفُسُوقُ بَعْدَ الايمَانِ وَمَن لَّمْ يَتُبْ فَأُوْلَئِكَ هُمُ الظَّالِمُونَ
“Wala msivunjiane hishima, wala msiitane kwa majina ya kejeli. Ni uovu kutumia jina baya baada ya kwisha amini. Na wasio tubu, hao ndio wenye kudhulumu”.
Al Hujurat - 11

Kuwasengenya watu, na maana yake ni kutafuta makosa yao na upungufu wao, na kuyazungumza kwa wengine.
Waislamu wanatakiwa wawe wenye kupendana mfano wa mwili mmoja, kila mmoja amsitiri mwenzake na sio kumfedhehesha.
Mwenyezi Mungu ِAnasema:
وَلا يَغْتَب بَّعْضُكُم بَعْضًا
“Wala msisengenyane nyinyi kwa nyinyi."
Al Hujurat - 12

Kwa hivyo Muislam anapomsengenya Muislam mwenzake au kumwita kwa jina ovu, anakuwa kama amejifanyia mwenyewe, na hii ni kwa sababu Muislam ni ndugu wa Muislam na Umma wa Kiislam ni Umma mmoja.
Katika mambo aliyoharamisha Mwenyezi Mungu, ni kujiamulia mambo kwa dhana tupu, kwa sababu dhana inaharibu uhusiano baina ya watu na kuwafanya watoe uamuzi kinyume na haki.

Mwenyezi Mungu ِAnasema:
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اجْتَنِبُوا كَثِيرًا مِّنَ الظَّنِّ إِنَّ بَعْضَ الظَّنِّ إِثْمٌ
“Enyi mlio amini! Jiepusheni na dhana nyingi, kwani baadhi ya dhana ni dhambi”.
Al Hujurat - 12

Mwenyezi Mungu ametukataza pia kupelelezana kutaka kujua siri za watu au kuona na kusikia yale ambayo wenyewe hawapendi wengine wayasikie.
Mwenyezi Mungu ِAnasema:
وَلا تَجَسَّسُوا
“Wala msipelelezane”.
Al Hujurat - 12
Katika kulifasiri neno ‘Kusengeya’ (Ghiyba), Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) aliwauliza Masahaba (Radhiya Llahu anhu):
"Mnajua nini maana ya kusengenya (Ghiyba)? "
Wakasema: "MwenyeziMungu na Mtume wake wanajua zaidi".
Akasema: "(Kusengenya) ni kuzungumza juu ya nduguyo (Muislam, akiwa hayupo) yale anayoyachukia".
Akaulizwa: "Je! ikiwa (ila) ninayoizungumzia anayo kweli?"
Akasema: "Ikiwa anayo kweli, basi huko ndiko kusengenya, na ikiwa si kweli, basi hayo ni madhambi makubwa zaidi (kwa kumsingizia uongo)”.
Muslim
Mwenyezi Mungu ametuwekea sheria na mafundisho mbali mbali katika mwenendo wetu na adabu zetu, na Muislam anatakiwa ayafuate. Miongoni mwa mafundisho hayo ni;
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amesema:
“Mwenye kumuamini Mwenyezi Mungu na Siku ya Kiama, amkirimu mgeni wake.”
Bukhari na Muslim
Katika mafundisho ya kiislamu ni kuomba ruhusa kabla ya kuingia majumbani mwa watu.
Mwenyezi Mungu anasema:
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لا تَدْخُلُوا بُيُوتًا غَيْرَ بُيُوتِكُمْ حَتَّى تَسْتَأْنِسُوا وَتُسَلِّمُوا عَلَى أَهْلِهَا ذَلِكُمْ خَيْرٌ لَّكُمْ لَعَلَّكُمْ تَذَكَّرُونَ
“Enyi mlio amini! Msiingie nyumba zisio nyumba zenu mpaka mwombe ruhusa, na mwatolee salamu wenyewe. Hayo ni bora kwenu mpate kukumbuka”.
An Nur – 27
Mwenyezi Mungu anasema:
وَإِذَا حُيِّيْتُم بِتَحِيَّةٍ فَحَيُّواْ بِأَحْسَنَ مِنْهَا أَوْ رُدُّوهَا إِنَّ اللّهَ كَانَ عَلَى كُلِّ شَيْءٍ حَسِيبًا
“Na mnapo amkiwa kwa maamkio yoyote, basi nanyi itikieni kwa yaliyo bora kuliko hayo, au rejesheni hayo hayo. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kuhisabu kila kitu”.
An Nisaa - 86

Na Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amesema:
“Haki ya Muislamu kwa mwenzake ni mambo matano;
1.   Kumtolea salaam,
2.   Kumtembelea anapoumwa,
3.   Kuhudhuria mazishi yake,
4.   Kuitikia wito anapokualika, na
5.   Kumwombea ndua anapokwenda chafya.
Bukhari na Muslim

Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) pia ametufundisha namna ya kutoa salam, akasema:
“Aliyepanda (gari, mnyama nk.) anamsalimia anayekwenda kwa miguu, (na) anayekwenda anamsalimia aliyekaa, watoto wawasalimie wakubwa na wachache wawasalimie wengi”.
Bukhari

Na akasema:
“Umtolee salamu unayemjua na usiyemjua”
Bukhari
Katika dini yetu tumefundishwa kusema; ‘Bismillahi’ kabla ya kula, na kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kusema; ‘Alhamdulillah’ baada ya kula, na pia tumefundishwa kula kwa mkono wa kulia.
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) alipomuona mtoto mdogo akila chakula ndani ya sinia , mara anakula kilicho chini yake na mara anakula kilicho mbali, akamwambia:
“Ewe kijana! Sema Bismillah, kula kwa mkono wa kulia na kula kilicho karibu yako’
Bukhari na Muslim

Tumefundishwa pia kuwa mtu anapokwenda chafya aseme: ‘Alhamdulillah’, na yule atakayemsikia (akisema Alhamdulillah) amwambie; ‘Yarhamuka Llah’, (Mwenyezi Mungu akurehemu). Kisha yule aliyepiga chafya anamjibu mwenzake kwa kumwambia; “Yahdiykumu Llahu wa yuslih baalakum”.(Mwenyezi Mungu akuhidi na astawishe hali yako).
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amesema:
"إذَا عَطَسَ أحَدُكُمْ فَلْيَقُل: الحَمْدُ لِلَّهِ، وَلْيَقُلْ لَهُ أخُوهُ أوْ صَاحبُهُ: يَرْحَمُكَ اللَّهُ، فإذَا قالَ لَهُ: يَرْحَمُكَ اللَّهُ، فَلْيَقُلْ: يَهْدِيكُمُ اللَّهُ وَيُصْلِحُ بالَكُمْ"
“Mmoja wenu akienda chafya aseme: ’Alhamdulillah’ na amjibu ndugu yake na rafiki yake (kwa kumwambia;) ‘Yarhamuka Llah’, na akimwambia; ‘Yarhamuka Llah’ amjibu kwa kumwambia: ‘Yahdiykumu Llahu wa yuslih baalakum”.
Bukhari
Katika mafundisho ya Kiislam pia tumekatazwa kunon’gona watu wawili ikiwa yupo wa tatu pamoja nao.
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amesema:
“Mnapokuwa watatu, wawili wasinon’gone wakamuacha wa tatu wao, mpaka mchanganyike na watu (muwe wengi) kwa sababu (kutenda) hivyo, kutamhuzunisha (wa tatu wenu)”.
Bukhari na Muslim
Dini yetu imetuamrisha na kupendekeza kuwazuru wagonjwa.
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amesema:
“Muislam anapomzuru ndugu yake Muislam, anakuwa ndani ya bustani za Peponi mpaka atakaporudi.”
Muslim
Ni vizuri pia mtu anapomtembelea mgonjwa na kabla ya kuondoka, asimame kuliani pake kisha aombe dua ifuatayo mara saba:
أسألُ اللَّهَ العَظِيمَ رَبّ العَرْشِ العَظِيمِ أنْ يَشْفِيكَ
“Namuomba Mola mtukufu Mola wa Arshi tukufu, akuafu”
Attirmidhy
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) ametukataza kula au kunywa tukiwa tumesimama wima.
Amesema Anas (Radhiya Llahu anhu):
“Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) ametukataza mtu kunywa akiwa amesima wima”. Anasema Qatada: ‘Tukamuuliza Anas; ‘Na kula je?’ Akasema; “Vibaya zaidi.”
Akimaanisha ‘kula wima’.
Muslim
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) ameharamisha mwanamume kuvaa dhahabu na vitambaa vya hariri.
Katika hadithi nyingi zilizomo katika Bukhari na Muslim na vitabu vingine sahihi kutoka kwa Masahaba mbali mbali (Radhiya Llahu anhum) wamesema:
“Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) ametukataza kuvaa dhahabu na hariri, na (ametukataza pia) kunywa ndani ya vyombo vya dhahabu na vya fedha, na akasema: “Vyombo hivi ni vyao hapa duniani na vyenu huko akhera”
Bukhari na Muslim
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) pia ametufundisha namna ya kuwalea watoto, kuwahurumia na kuwabusu.
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) alikuwa akiwabusu Al Hassan na Al Hussein (Radhiya Llahu anhum), na alimkataza yule aliyesema kuwa ana watoto kumi na hajapata kumbusu yeyote kati yao hata siku moja. Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) alimwambia:
“Asiyekuwa na huruma, hatohurumiwa.”
Bukhari
Rehma ya Muislam si kwa ajili kwa wanadamu peke yao, bali tumeamrishwa kuwahurumia hata wanyama.
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) alitujulisha juu ya yule aliyekuwa na kiu, na baada ya kunywa maji kisimani akamuona mbwa akihangaika mbele ya kisima, akajisemea moyoni mwake:
“Bila shaka mbwa huyu ana kiu kikubwa”. Akachota maji kisimani na kumnywesha. Mwenyezi Mungu akamghufiria madhambi yake yote.
Masahaba (Radhiya Llahu anhu) waliposikia hayo wakamuuliza:
“Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, hata katika wanyama tunapata thawabu?”
Akasema:
“Katika kila kiumbe kilicho hai mnapata thawabu (mkikifanyia wema na kukihurumia).
Bukhari

Upole
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) ametufundisha kuwa wapole na wavumilivu katika kutatua matatizo yetu. Alimfundisha Bibi Aisha (Radhiya Llahu anhu) hayo pale Bibi Aisha alipowatukana Mayahudi na kuwalani. Akamwambia:
“Taratibu ewe Aisha, Mwenyezi Mungu anapenda upole katika kila kitu”
Bukhari
Kisa chenyewe kilikuwa hivi:
Liliingia kundi la Mayahudi kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) na badala ya kumtolea salaam kwa kumuambia "ASSALAAM alaykum, wakamuambia:
“ASSAAM aleikum”, na maana yake NI; “Mauti yawe juu yenu.”
Walisema hivyo wakidhania kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) hatotambua. Lakini Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) akawajibu:
“Wa alaikum”. Bila ya kuongeza neno lolote, na maana yake; “Na juu yenu pia”.
Bibi Aisha (Radhiya Llahu anha) aliyekuwa amekaa pamoja na Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) wakati ule akawajibu kwa ghadhabu:
‘Alaykumu assaam wa Llaana’
“Mauti yawe juu yenu pamoja na laana”
Ndipo Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) alipomwambia:
“Taratibu ewe Aisha, Mwenyezi Mungu anapenda upole katika kila kitu.”
Anasema Bibi Aisha (Radhiya Llahu anha):
“Nikamwambia: "Hukuwasikia walivyosema?”
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) akanijibu:
“Nimesikia, ndio maana nikawajibu ‘Wa aleikum”
Na maana yake “Na juu yenu”
Mwenyezi Mungu ametuamrisha tusaidiane wenyewe kwa wenyewe kwa wema na kwa uchaMungu, akasema:
وَتَعَاوَنُواْ عَلَى الْبرِّ وَالتَّقْوَى وَلاَ تَعَاوَنُواْ عَلَى الإِثْمِ وَالْعُدْوَانِ
“Na saidianeni katika wema na uchamungu. Wala msisaidiane katika dhambi na uadui”.
Al Maidah – 2
Na Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amefananisha kushikamana kwa Waislam kuwa sawa na kushikamana kwa mwili mmoja, na akafananisha kushikamana huko kuwa ni sawa na kushikamana kwa majengo.
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amesema:
“Waislam katika kuhurumiana kwao na kupendana kwao na kupendeleana kwao ni mfano wa mwili mmoja, kinaposikitika kiungo (chochote kwa kuumwa), basi mwili wote unashirikiana katika kukesha na kupata homa”.
Bukhari na Muslim
Na katika hadithi nyingine amesema:
“Waislam ni mfano wa majengo, yameshikamana na kuzuwiana yenyewe kwa yenyewe (yasianguke)”.
Bukhari
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) ametuhadharisha juu ya tabia mbaya sana ya 'Namiyma', nayo ni mtu kuchukua maneno ya huku na kuyapeleka kule kwa nia ya kufitinisha.
Siku moja Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) alipopita karibu na kaburi, aliwajulisha Masahaba (Radhiya Llahu anhum) kuwa mwenye kaburi lile anaadhibishwa kwa sababu alikuwa akiishi baina ya wenzake akiwa na tabia hiyo ovu.
Uislam unatufundisha pia ubora wa kusaidia watu na kukidhi haja zao.
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amesema:
“Anayejishughulisha na kuwasaidia ndugu zake, na Mwenyezi Mungu atamsaidia. Na atakayemuondolea Muislam mwenzake dhiki yake, basi Mwenyezi Mungu atamuondolea dhiki katika dhiki zake za Siku ya Kiama. Na atakayemsitiri Muislam na Mwenyezi Mungu atamsitiri Siku ya Kiama”.
Muslim
Tabia, ni ule mwenendo alio nao mwanadamu ndani ya nafsi yake. Mwenendo ambao si rahisi mtu kuweza kuubadilisha, kwa sababu chimbuko lake ni ndani ya nafsi yake, na hatimaye unageuka mwenendo huo kuwa ni sehemu ya dhati yake asiyoweza kuachana nayo.
Baadhi ya maulama wa elimu ya nafsi wanasema kuwa Tabia ya mtu ni mfano wa picha yake ikikuelezea ni nani yeye, na anaweza kujulikana mtu undani wake kutokana na tabia zake.
Bila shaka tabia ziko ovu na ziko njema.

Katika lugha ya kiarabu neno ‘Khalqu’ maana yake “Umbile” na neno “Khuluqu” maana yake “Tabia”. La mwanzo kwa kutumia ‘a’ ‘Khalqu’ na linatujulisha juu ya umbile la nje la kiumbe. Ama la pili kwa herufi ‘u’ ‘Khuluqu’ linatujulisha juu ya umbile la ndani la kiumbe.
Kwa hivyo neno ‘Khalqu’ (Umbile), linamaanisha sura inayo onekana ya kiumbe na neno ‘Khuluqu’ ambalo kwa kiswahili tunaita ‘Khuluka’ na maana yake ni tabia, linatujulisha juu ya zile tabia ambazo si kitu cha kuonekana kwa jicho, bali zimo ndani ya nafsi yake mwanadamu.
Kama tulivyoandika hapo mwanzo kuwa Tabia ziko aina mbili; Njema na Ovu.
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) alimuambia Ash'aj Abdul Qais (Radhiya Llahu anhu):
“Una mambo mawili ambayo Mwenyezi Mungu anayapenda; Upole na Kutokuwa na pupa”.
Ahmed – Annasai – na Bukhari katika Adabul mufrad (Fathu l Bari)
Miongoni mwa tabia njema, ni Kusema kweli, Uaminifu, Ukarimu, Kutimiza Ahadi, Ushujaa na Subira. Bila shaka mwenye tabia hizi anastahiki kukirimiwa na kupewa kila sifa anayostahiki.
Miongoni mwa Tabia ovu ni; Kusema Uwongo, Khiana, Uwoga, na Kusengenya.
Mwenye tabia hizi, bila shaka anastahiki kila lawama.
Mwenyezi Mungu ametuwekea sheria inayowaita (inayowalingania) watu katika Tabia njema na kuwakataza Tabia ovu, ili nafsi zipate kutahirika na kutakasika na ili watu waweze kuishi vizuri baina yao.
Kwa ajili hii, utaona kuwa mafundisho mengi ya dini yamezungumzia maudhui haya na hayakuacha kumpa sifa anazostahiki kila mwenye tabia njema. Inatosha kauli yake Suhanahu wa Taala alipomsifia Mtume wake kwa kumwambia:
وَإِنَّكَ لَعَلى خُلُقٍ عَظِيمٍ
“Na bila shaka una tabia njema kabisa”.
Suratul Qalam - 4

Mwenyezi Mungu akatutaka pia tuzikimbilie Rehema Zake na Pepo Yake aliyowatayarishia wacha Mungu katika waja wake wenye sifa hiyo ya Tabia njema.
Mwenyezi Mungu ِِAnasema:
وَسَارِعُواْ إِلَى مَغْفِرَةٍ مِّن رَّبِّكُمْ وَجَنَّةٍ عَرْضُهَا السَّمَاوَاتُ وَالأَرْضُ أُعِدَّتْ لِلْمُتَّقِينَ. الَّذِينَ يُنفِقُونَ فِي السَّرَّاء وَالضَّرَّاء وَالْكَاظِمِينَ الْغَيْظَ وَالْعَافِينَ عَنِ النَّاسِ وَاللّهُ يُحِبُّ الْمُحْسِنِينَ
“Na yakimbilieni maghfira ya Mola wenu Mlezi, na Pepo ambayo upana wake tu ni sawa na upana wa mbingu na ardhi, iliyo wekwa tayari kwa wachamungu.
Ambao hutoa wanapo kuwa na wasaa na wanapo kuwa na dhiki, na wanajizuia
ghadhabu, na wasamehevu kwa watu; na Mwenyezi Mungu huwapenda wafanyao wema.”
Aal Imran – 133-134
Na katika aya ifuatayo, Mwenyezi amewasifia wenye kutimiza ahadi, wavumilivu wakati wa shida, wakati wa madhara na wakati wa vita, kuwa ni watu wenye Tabia njema.
Mwenyezi Mungu Anasema:

لَّيْسَ الْبِرَّ أَن تُوَلُّواْ وُجُوهَكُمْ قِبَلَ الْمَشْرِقِ وَالْمَغْرِبِ وَلَـكِنَّ الْبِرَّ مَنْ آمَنَ بِاللّهِ وَالْيَوْمِ الآخِرِ وَالْمَلآئِكَةِ وَالْكِتَابِ وَالنَّبِيِّينَ وَآتَى الْمَالَ عَلَى حُبِّهِ ذَوِي الْقُرْبَى وَالْيَتَامَى وَالْمَسَاكِينَ وَابْنَ السَّبِيلِ وَالسَّآئِلِينَ وَفِي الرِّقَابِ وَأَقَامَ الصَّلاةَ وَآتَى الزَّكَاةَ وَالْمُوفُونَ بِعَهْدِهِمْ إِذَا عَاهَدُواْ وَالصَّابِرِينَ فِي الْبَأْسَاء والضَّرَّاء وَحِينَ الْبَأْسِ أُولَـئِكَ الَّذِينَ صَدَقُوا
“Sio wema kuwa mnaelekeza nyuso zenu upande wa Mashariki na Magharibi. Bali wema ni wa anaye muamini Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho na Malaika na Kitabu na Manabii, na anawapa mali kwa kupenda kwake, jamaa na mayatima na masikini na wasafiri, na waombao, na katika ugombozi, na akawa anashika Sala, na akatoa Zaka, na wanao timiza ahadi yao wanapo ahidi, na wanao vumilia katika shidana dhara na wakati wa vita; hao ndio walio sadikisha, hao ndio wajilindao.”
Al Baqarah – 177

Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) pia ametufundisha mengi juu ya umuhimu wa kuwa na Tabia njema.
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amesema:
“Wema (kutenda mema) ni (katika) Tabia njema”.
Muslim

Na akasema:
“Mbora wenu ni yule mwenye Tabia njema zaidi”.
Bukhari

Na akasema:
“Kwa hakika, Muislam mkamilifu wa Imani ni yule mwenye Tabia njema kupita wenzake”
Attirmidhiy na Al Hakim

Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) pia ametujulisha kuwa Tabia njema ndiyo yenye uzito zaidi juu ya mizani Siku ya Kiama.
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amesema:
“Hakuna chenye uzito zaidi juu ya mizani kuliko Tabia njema”
Bukhari, Abu Daud, Attirmidhiy na imesahihishwa na Ibni Hibban

Tabia njema pia ni katika sababu kubwa za kuingizwa katika Pepo ya Mwenyezi Mungu.
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) alipoulizwa juu amali gani zinazowaingiza watu zaidi Peponi akasema:
“Ucha Mungu na Tabia njema”
Attirmidhiy na Ibni Hibban (Bukhari katika Fathi l Bari)

Na akasema:
“Katika wale ninaowapenda sana miongoni mwenu na watakaokuwa karibu nami Siku ya Kiama, ni wale wenye Tabia njema, na katika wale ninaowachukia na watakaokuwa mbali zaidi nami, ni wale wenye kusema maneno mengi yasiyo na maana na wenye kuzungumza kwa kujinata (huku akiukaza ulimi na kuuregeza na kujifanya kuwa yeye ni mfasihi kuliko wenzake) na wenye kuzungumza kwa kiburi.”
Attirmidhiy

Bila shaka mwenye Tabia na mwenendo mwema pamoja na maneno mazuri yasiyo na kiburi, ni mwenye kupendeka zaidi mbele ya wenzake.
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amesema:
“Hamtopendwa na watu kwa ajili ya mali zenu, bali mtapendwa kwa ajili ya ukunjufu wa nyuso zenu na Tabia zenu njema”.
Al Bazzaar
Tumesoma hapo mwanzo kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) ni mfano bora wa kufuatwa katika Tabia njema, hata Mola wake Subhaanahu wa Taala Akamuambia:
وَإِنَّكَ لَعَلى خُلُقٍ عَظِيمٍ
“Na bila shaka una tabia njema kabisa”.
Suratul Qalam - 4

Masahaba wake (Radhiya Llahu anhum) na adui zake, wote walikubaliana juu ya Tabia zake njema. Hajawahi hata siku moja yeyote katika adui zake kumtuhumu Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) kuhusu jambo hili, bali Tabia zake njema zilijulikana kila pembe ya dunia.
Anas bin Malik (Radhiya Llahu anhu) alimtumikia Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) miaka kumi, na alikuwa hambanduki kila anapokwenda, na kwa ajili hiyo bila shaka alikuwa akimjua vizuri sana Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam).
Tumsikilize nini anasema juu ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam):
Anasema Anas (Radhiya Llahu anhu):
“Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) alikuwa mbora wa viumbe, mkarimu kupita wote na alikuwa shujaa kupita wote”.
Anaendelea kusema:
“Nimemtumikia Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) miaka kumi, wallahi hajapata hata siku moja kuniambia:”Ah!”, na wala hajapata kuniambia kuhusu jambo lolote nililofanya: ”Kwa nini umefanya," au "bora ungefanya hivi”.
Muslim
Mwenyezi Mungu Subhanahu wa Taala kama alivyozisifia Tabia njema, pia amezilaumu Tabia ovu pamoja na wenye tabia hizo.
Mwenyezi Mungu ِِِAnasema:
وَلا تُطِعْ كُلَّ حَلافٍ مَّهِينٍ. هَمَّازٍ مَّشَّاء بِنَمِيمٍ. مَنَّاعٍ لِّلْخَيْرِ مُعْتَدٍ أَثِيمٍ
“Wala usimt'ii kila mwingi wa kuapa wa kudharauliwa.
Mtapitapi, apitaye akifitini. Mwenye kuzuia kheri, dhaalimu, mwingi wa madhambi.
Mkavu, na juu ya hayo, mshari, amejipachika tu.”
Al Qalam – 10 - 13

Katika kumkataza mwanawe tabia mbovu, Luqmaan mwenye hekima alisema:

وَلا تُصَعِّرْ خَدَّكَ لِلنَّاسِ ولا تَمْشِ فِي الْأَرْضِ مَرَحًا إِنَّ اللَّهَ لا يُحِبُّ كُلَّ مُخْتَالٍ فَخُورٍ
“Wala usiwabeuwe watu, wala usitembee katika nchi kwa maringo. Hakika Mwenyezi Mungu hampendi kila anaye jivuna na kujifakhirisha.”
Luqman – 18
Baadhi ya wataalam wanasema kuwa; Tabia ni mizizi iliyo ndani ya nafsi ya mtu. Ni kitu alichoumbwa nacho, na kwamba haiwezekani mtu kujirekebisha au hata kujaribu kuzibadilisha tabia zake. Baadhi ya watu wakapata kisingizio kutokana na msemo huu, wakaona uzito kujitahidi katika kuzirekebisha tabia zao.
Lakini ukweli ni kwamba zipo katika Tabia njema ambazo mtu ameumbwa nazo ndani ya nafsi yake. Na mtu anapojaaliwa na kitu kama hicho, amshukuru Mwenyezi Mungu aliyempa fadhila hizo.
Wakati huo huo zipo tabia njema ambazo mtu huzipata kwa kujaribu na kujitahidi, kama tulivyoona katika ile hadithi ya Al Ash'aj wakati Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) alipomwambia:
“Una mambo mawili ambayo Mwenyezi Mungu anayapenda; Upole na Kutokuwa na pupa”.
Al Ash'aj, akamuuliza Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam):
“Ninazo (tabia hizo) tokea mwanzo (nimezaliwa nayo) au nimezipata baadaye?”
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) akamjibu:
“Tokea mwanzo”
Akasema:
“Namshukuru Mwenyezi Mungu aliyeniumba na tabia mbili anazozipenda”.
Ahmed – Annasai – na Bukhari katika Adabul mufrad (Fathu l Bari).
Katika kuisherehesha hadithi hii, anasema Ibni Hajar Al Asqalani, mmoja wa Maulamaa wakubwa wa Kiislam:
“Kutokana na jawabu ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam), tunaelewa kuwa zipo katika Tabia mtu ameumbwa nazo, na zipo zile ambazo mtu anaweza kuzipata au kujifunza”.
Fathi l Bari

Zipo dalili nyingi zinazothibitisha kuwa mtu anaweza kuzipata au kujifunza.Tabia njema:

Kwanza:-
Tunaona kwa mfano mtu mwoga, kutokana na kupewa mafunzo mengi na jitihada nyingi anageuka kuwa shujaa. Na pia tunaona mara nyingine mtu mwongo, kwa mafunzo na malezi bora, anageuka kuwa ni msema kweli. Kama vile tulivyoona wagomvi na watu waovu, baada ya kumjua Mola wao na kuongezeka imani yao, wanageuka kuwa ni watu wema, na wakati huo huo tunaona watu wema wanapochanganyika na watu waovu kwa muda mrefu, wao nao wanageuka kuwa watu waovu.

Pili:-
Tumeona pia mara nyingi wanyama wanapopata mafunzo, hubadilisha Tabia zao. Tumeona kwa mfano paka anapopata mafunzo maalum, huishi pamoja na mapanya, na mbwa anaishi na paka, na pia tumeona kima wanapopata mafunzo maalum huweza kufanya mambo mengi ya kiajabu. Ikiwa mwenendo wa wanyama unaweza kubadilika, basi uwezo wa mwanadamu ni mkubwa zaidi.
Tatu:-
Mweyezi Mungu katika sehemu nyingi ametutaka tuzibadilishe tabia zetu na kuwa na Tabia njema.
Mwenyezi Mungu ِِAnasema:
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُواْ اتَّقُواْ اللّهَ وَكُونُواْ مَعَ الصَّادِقِينَ
“Enyi mlio amini! Mcheni Mwenyezi Mungu, na kuweni pamoja na wakweli.”
At Tawba – 119

Na Akasema:
وَاصْبِرْ وَمَا صَبْرُكَ إِلاَّ بِاللّهِ وَلاَ تَحْزَنْ عَلَيْهِمْ وَلاَ تَكُ فِي ضَيْقٍ مِّمَّا يَمْكُرُونَ
“Na subiri. Na kusubiri kwako kusiwe ila kwa sababu ya Mwenyezi Mungu tu. Wala usiwahuzunikie; wala usiwe katika dhiki kwa hila wanazo zifanya.”
An Nahl-127

Na Akasema:
وَأَنفِقُواْ فِي سَبِيلِ اللّهِ وَلاَ تُلْقُواْ بِأَيْدِيكُمْ إِلَى التَّهْلُكَةِ وَأَحْسِنُوَاْ إِنَّ اللّهَ يُحِبُّ الْمُحْسِنِينَ
“Na toeni katika njia ya Mwenyezi Mungu, wala msijitie kwa mikono yenu katika maangamizo. Na fanyeni wema. Hakika Mwenyezi Mungu huwapenda wafanyao wema.”
Al Baqarah - 195

Ingelikuwa Tabia za mtu haziwezi kubadilika, basi amri za Mwenyezi Mungu pale anapotutaka tubadilishe Tabia zetu na kuzifanya ziwe njema zitakuwa hazileti maana. Na kila mwenye akili timamu anatambua kuwa Mwenyezi Mungu haamrishi jambo lisilo na maana wala haamrishi yale tusiyoyaweza.
Mwenyezi Mungu Anasema:
لاَ يُكَلِّفُ اللّهُ نَفْسًا إِلاَّ وُسْعَهَا لَهَا مَا كَسَبَتْ وَعَلَيْهَا مَا اكْتَسَبَتْ رَبَّنَا لاَ تُؤَاخِذْنَا إِن نَّسِينَا أَوْ أَخْطَأْنَا رَبَّنَا وَلاَ تَحْمِلْ عَلَيْنَا إِصْرًا كَمَا حَمَلْتَهُ عَلَى الَّذِينَ مِن قَبْلِنَا رَبَّنَا وَلاَ تُحَمِّلْنَا مَا لاَ طَاقَةَ لَنَا بِهِ وَاعْفُ عَنَّا وَاغْفِرْ لَنَا وَارْحَمْنَآ أَنتَ مَوْلاَنَا فَانصُرْنَا عَلَى الْقَوْمِ الْكَافِرِينَ
“Mwenyezi Mungu haikalifishi nafsi yoyote ila kwa kadiri iwezavyo. Faida ya iliyo yachuma ni yake, na khasara ya iliyo yachuma ni juu yake pia. (Ombeni:)Mola wetu Mlezi! Usituchukulie tukisahau au tukikosea. Mola wetu Mlezi! Usitubebeshe mzigo kama ulio wabebesha wale walio kuwa kabla yetu. Mola wetu Mlezi Usitutwike tusiyo yaweza, na utusamehe, na utughufirie, na uturehemu. Wewe ndiye Mlinzi wetu. Basi tupe ushindi tuwashinde kaumu ya makafiri.”
Al Baqarah - 286

Nne:-
Katika hadithi sahihi, Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amesema:
“Hakika ya elimu (mtu huipata) kwa kujifunza, na upole (mtu hujifunza) kwa kuwa mpole na mtu anapoitafuta kheri ataipata, na anayejiepusha na shari, huepushwa nayo.”
Al Khatib, kutoka kwa Abi Huraira
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) pia alikuwa akimuomba Mwenyezi Mungu amuongoze katika Tabia njema.
Katika dua ya kufungulia sala alikuwa akiomba kwa kusema:
واهدني لأحسن الأخلاق لا يهدي لأحسنها إلا أنت واصرف عني سيئها لا يصرف عني سيئها إلا أنت
Na maana yake ni;
“Na uniongoze katika Tabia njema, hapana aongozae katika Tabia njema isipokuwa Wewe. Na uniepushe na Tabia mbaya, hapana anaye epusha nazo isipokuwa Wewe.”
Muslim, Attirmdhy Annasai na wengine
Mmoja katika maulamaa wa India aitwae Muhammad Yaaqub Al Fairuz Abadiy amezigawa Tabia njema katika sehemu nne zifuatazo;
1.           Subira
2.           Wema
3.           Ushujaa
4.           Uadilifu

1.           Mwenye Subira kwa kawaida huwa mstahamilivu. Hupenda kuwaondolea wenzake udhia, huwa mwenye huruma, mpole, na kwa kawaida mweye Subira hawi na tabia ya pupa na uamuzi wa haraka.
2      Mtu Mwema daima hujiepusha na utovu wa adabu na uovu katika vitendo na matamshi, na pia huwa mwingi wa haya. Na tabia hii ya kuona haya ni nguzo muhimu sana katika mambo ya kheri.
Wema pia humuepusha mtu na matendo machafu, ubakhili, uwongo, kusengenya na kufitinisha watu kwa kuchukua maneno ya huku na kuyapeleka kule.
3      Mtu Shujaa kwa kawaida hujiheshimu. Hapendi kuwakosea wenzake kama vile yeye alivyokuwa hapendi kukosewa. Shujaa pia huwa na tabia ya kuwatakia wenzake kheri, hata kama yeye atakosa, na huwa na uwezo wa kuzuwia ghadhabu zake na kwa kawaida huwa mpole.

Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amesema:
“Ushujaa si kwa uhodari wa kupigana mieleka, bali ushujaa ni mtu anayeimiliki nafsi yake wakati wa ghadhabu”.
Huu ndio ushujaa, nao ni ufalme na hawezi kuumiliki ufalme huo isipokuwa Shujaa peke yake.
4      Uadilifu, kama alivyosema Feiruz Abadi; Humfanya mwenye tabia hiyo kuweza kufanya mambo yake yote kwa Uadilifu, kati na kati bila ya kupindukia mipaka katika kutoa wala katika kuzuwia nk.
Ukweli ndiyo njia ya ushindi na mafanikio, na uwongo ndiyo njia ya kushindwa na upotofu. Hivi ndivyo dini yetu inavyotufundisha na hivi ndivyo ilivyothibiti katika maisha yetu na matendo yetu ya siku zote.
Kama yupo mwenye kudhania kinyume cha hayo, basi amekosea. Akiwepo anayedhania kuwa uwongo ndio utakaomuokoa, na ukweli utamuangamiza, basi huyo bado hajaijua vizuri haki na yuko mbali nayo kabisa.
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) ametufundisha hayo katika hadithi iliyosimuliwa na Abdillahi bin Masaood (Radhiya Llahu anhu).
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amesema:
“Shikamaneni na ukweli, kwa sababu ukweli unaongoza katika wema, na wema kwa hakika unaongoza katika Pepo, na mtu anaposema kweli na akawa anajilazimisha (kila anaposema) kusema kweli, mpaka ataandikwa kwa MwenyeziMungu kuwa ni Msemakweli. Na jiepusheni na uwongo, kwa sababu uwongo kwa hakika unaongoza katika maovu, na maovu kwa hakika yanaongoza katika Moto. Na mtu anaposema uwongo, na akawa anajilazimisha (kila anaposema) kusema uwongo, mpaka ataandikwa kwa Mwenyezi Mungu kuwa kuwa ni Muongo”.
Bukhari na Muslim

Zifuatazo ni sifa walizopewa waliosadiki na kuamini kikweli:
Mwenyezi Mungu ِAnasema:
مِنَ الْمُؤْمِنِينَ رِجَالٌ صَدَقُوا مَا عَاهَدُوا اللَّهَ عَلَيْهِ فَمِنْهُم مَّن قَضَى نَحْبَهُ وَمِنْهُم مَّن يَنتَظِرُ وَمَا بَدَّلُوا تَبْدِيلا
“Miongoni mwa Waumini wapo watu walio timiza waliyo ahidiana na Mwenyezi Mungu.Baadhi yao wamekwisha kufa, na baadhi wanangojea, wala hawakubadilisha (ahadi) hata kidogo.”
Al Ahzab – 23

Wale waliokadhibisha na kutoa ahadi za uwongo, Mwenyezi Mungu Amesema juu yao:
وَمِنْهُم مَّنْ عَاهَدَ اللّهَ لَئِنْ آتَانَا مِن فَضْلِهِ لَنَصَّدَّقَنَّ وَلَنَكُونَنَّ مِنَ الصَّالِحِينَ. فَلَمَّا آتَاهُم مِّن فَضْلِهِ بَخِلُواْ بِهِ وَتَوَلَّواْ وَّهُم مُّعْرِضُونَ. فَأَعْقَبَهُمْ نِفَاقًا فِي قُلُوبِهِمْ إِلَى يَوْمِ يَلْقَوْنَهُ بِمَا أَخْلَفُواْ اللّهَ مَا وَعَدُوهُ وَبِمَا كَانُواْ يَكْذِبُونَ
“Na miongoni mwao wapo walio muahidi Mwenyezi Mungu kwa kusema: Akitupa katika fadhila yake hapana shaka tutatoa sadaka, na tutakuwa katika watendao mema.
Alipo wapa katika fadhila yake wakaifanyia ubakhili na wakageuka, na huku
Wakipuuza, basi akawalipa unafiki kuutia nyoyoni mwao mpaka Siku watapo kutana naye, kwa sababu ya kuwa walimkhalifu Mwenyezi Mungu katika yale waliyo muahidi, na kwa sababu ya kusema kwao uwongo.”
At Tawba – 75-77

'Ukweli', kama unavyotakiwa katika mazungumzo na katika kutimiza ahadi, pia unatakiwa katika matendo. Kwa sababu mtu anapoahidi kutenda jambo, kwa mfano anapomuahidi Mwenyezi Mungu kutoa sadaka atakapojaaliwa kupata pesa, basi wakati unapowadia lazima aitimize ahadi hiyo. Na siku zote mtu anatakiwa ajitahidi katika kuudhihirisha ukweli katika kauli zake na matendo yake, ili matendo hayo yadhihirishe yale yaliyo ndani ya nafsi yake.
Msema kweli siku zote hupendeza mbele ya watu. Wanamuaminisha hata mali zao. Ushahidi wake unakubaliwa na unakuwa na uzito mbele ya wenzake. Kinyume na muongo ambaye watu hawamsadiki, na ushahidi wake haukubaliwi, na watu hawamuamini katika mali zao.
Atakayejichunguza akaijua asili yake aliyoumbiwa na Mwenyezi Mungu, akauchunguza ulimwengu aliyezaliwa na kukuwa ndani yake, kisha akamjua Mola wake mtukufu aliyemuumba yeye na aliyeumba ulimwengu wote, itambidi aondoe majivuno yake, na amsitahi Mola wake mtukufu. Kustahi huko, kutaonekana matunda yake katika kauli zake anazotamka na katika matendo yake.
Tumsikilize Mwenyezi Mungu Akituelezea juu ya waja wake wasiokuwa na majivuno.
Mwenyezi Mungu Anasema:
وَعِبَادُ الرَّحْمَنِ الَّذِينَ يَمْشُونَ عَلَى الاَرْضِ هَوْنًا وَإِذَا خَاطَبَهُمُ الْجَاهِلُونَ قَالُوا سَلامًا
“Na waja wa Arrahman (Mwingi wa Rehema) ni wale wanao tembea ulimwenguni kwa staha, na wajinga wakiwasemeza hujibu: Salama!”.
Al Furqan - 63

Kiburi kinatokana na ujinga wa mtu asiyeijuwa kadiri yake na asiyeijuwa kadiri ya Mola wake aliyemuumba. Kwa sababu kila kitu hapa duniani ni cha kupita, hakina thamani yoyote na hakistahiki mtu kutakabari kwa ajili yake.
Pesa zitaondoka, ufalme utaondoka, uzuri utatoweka na uhai haudumu milele. Hapana atakayebaki isipokuwa Mwenyezi Mungu peke yake.
Mwenyezi Mungu Anasema:
كُلُّ مَنْ عَلَيْهَا فَانٍ. وَيَبْقَى وَجْهُ رَبِّكَ ذُو الْجَلالِ وَالإكْرَامِ
“Kila kilioko juu yake kitatoweka.”
Na atabakia Mwenyewe Mola wako Mlezi Mwenye utukufu na ukarimu.”
Ar Rahman – 26 – 27

Kwa hivyo mwenye kiburi anajipachika cheo asichostahiki. Anashindana na Mola wake katika moja wapo ya sifa Zake, na Mwenyezi Mungu haridhiki na jambo hilo.
Katika Hadithul Qudusiy, Mwenyezi Mungu anasema:
“Kiburi ni (mfano wa) vazi langu la chini, na utukufu ni (mfano wa) vazi langu la juu atakaye (jaribu) kuninya’nganya moja kati ya hizo, nitamtupa Motoni na wala sijali.”
Muslim
Mwenye kiburi hawezi kufaidika na wenye kuilingania haki, kwa sababu kiburi chake kinamzuwia asiweze kuikubali haki, na matokeo yake hupata hasara kubwa.
Mwenyezi Mungu anasema:
سَأَصْرِفُ عَنْ آيَاتِيَ الَّذِينَ يَتَكَبَّرُونَ فِي الأَرْضِ بِغَيْرِ الْحَقِّ وَإِن يَرَوْاْ كُلَّ آيَةٍ لاَّ يُؤْمِنُواْ بِهَا وَإِن يَرَوْاْ سَبِيلَ الرُّشْدِ لاَ يَتَّخِذُوهُ سَبِيلاً وَإِن يَرَوْاْ سَبِيلَ الْغَيِّ يَتَّخِذُوهُ سَبِيلاً ذَلِكَ بِأَنَّهُمْ كَذَّبُواْ بِآيَاتِنَا وَكَانُواْ عَنْهَا غَافِلِينَ
“Nitawatenga na Ishara zangu wale wanao fanya kiburi katika nchi bila ya haki. Na wao wakiona kila Ishara hawaiamini. Wakiiona njia ya uwongofu hawaishiki kuwa ndiyo njia; lakini wakiiona njia ya upotofu wanaishika kuwa ndiyo njia. Hayo ni kwa sababu wamezikanusha Ishara zetu, na wameghafilika nazo.”
Al Aaraf- 146

Na mwenye kiburi hupata hasara ya nafsi yake, kwa sababu yeyote mwenye sifa ya kuwa na kiburi, Mwenyezi Mungu humdhalilisha.
Mwenyezi Mungu Anasema:
إِنَّ الَّذِينَ يَسْتَكْبِرُونَ عَنْ عِبَادَتِي سَيَدْخُلُونَ جَهَنَّمَ دَاخِرِينَ
“Kwa hakika wale ambao wanajivuna na kuniabudu Mimi wataingia Jahannamu wadhalilike”.
Ghafir (Al Muuminun) – 60

Mwenyezi Mungu anamdhalilisha mwenye kiburi, lakini wakati huo huo asiye na kiburi Mwenyezi Mungu humtukuza na kumkirimu.
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) anasema:
“Mwenyezi Mungu humuongezea utukufu mja wake anayesamehe, na mtu anapoondowa kiburi chake mbele ya Mwenyezi Mungu, basi Mwenyezi Mungu humnyanyua”.
Muslim

Al Fudhail bin Abbas amemuelezea asiye na kiburi kuwa na sifa zifuatazo;
“Mwenye kuikubali haki na kuifuata. Hata ukiisikia kutoka kwa asiyekuwa na elimu, (haki) lazima uikubali”.
Kitabu ‘Tahadhiyb mauidhatul Muuminin’

Lakini kiburi ni kinyume na hivyo. Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amesema:
“Kiburi ni kuipinga haki na kuwadharau watu”.
Muslim
Wafuasi wa dini zote wanajulikana kwa sifa zao maalum. Sifa ambazo wasiokuwa wao hawana. Kwa mfano Mayahudi wanajulikana kuwa wana sifa ya khofu, Manasara, wana sifa ya kupenda. Ama Waislamu, wao wana sifa ya aina yao peke yao, nayo ni mchanganyiko wa khofu na kupenda, nayo ni kuona haya.
Katika kitabu chake Imam Malik kiitwacho Al Muwata- a anasema:
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amesema:
“Kila dini ina khuluqa zake, na khuluqa za Uislamu ni kuona haya”.
Khuluqa njema inamuongoza mtu katika kufanya amali njema, lakini khuluqa mbaya inamuongoza mtu katika maovu. Kwa hivyo anayemsitahi Mwenyezi Mungu, hupenda kumtii, na kuepukana na kumuasi pamoja na kumuabudu kama anavyopaswa kuabudiwa.
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amesema:
“Msitahini Mwenyezi Mungu kama anavyopaswa kustahiwa”
Attirmidhy
Na akasema:
“Kuona haya hakuleti (kingine) isipokuwa kheri tupu”.
Bukhari na Muslim

Na kuona haya ni dalili ya kuwa na imani.
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amesema:
“Imani ina sehemu sabini na zaidi. Sehemu ya juu kabisa ni kauli ya ‘La ilaaha illa Llah’ na ya chini ni kuondoa udhia barabarani, na kuona haya ni sehemu katika sehemu za imani”.
Bukhari na Muslim

Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) siku moja alipokuwa akipita njiani, alimsikia mtu akimnasihi ndugu yake apunguze kuona haya, Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) akamwambia:
“Mwache, kwani kuona haya ni dalili ya kuwa na imani”.
Bukhari na Muslim

Ikiwa kuona haya kunamsaidia mtu katika matendo ya kheri, kwa hivyo kutokuwa na haya kunaondoa vile vikwazo vinavyomfanya mtu asitende maovu na kumfanya ateleze na kuanza kuyatenda maovu hayo.
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amesema:
“Katika maneno yaliyonukuliwa kutoka kwa Mitume iliyotangulia; (ni haya yafuatayo): “Ikiwa huna haya, basi tenda utakalo”.
Bukhari

Juu ya kuwa kuona haya ni jambo la kheri, lakini haya hizo zisimpeleke mtu akaacha kufanya matendo mema, kukakataza maovu na kuuliza katika mambo ya dini yale asiyoyaelewa.
Ummu Salama (Radhiya Llahu anha) amesema kumwambia mumewe Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam):
“Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, hakika Mwenyezi Mungu Hatutaki tuone haya katika (kuijua) haki, je! Mwanamke anapoota anatakiwa kukoga?”
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) akasema: “Ndiyo, atakapoyaona maji”
Bukhari
Kupendelea, nako ni mtu kumpendelea kheri mwenzake kuliko nafsi yake. Na hii ni daraja kubwa isiyoweza kufikiwa isipokuwa na watu wenye daraja kubwa. Masahaba (Radhiya Llahu anhum) walizifikia daraja hizo, na Mwenyezi Mungu ameshuhudia hayo pale Aliposema:
وَيُؤْثِرُونَ عَلَى أَنفُسِهِمْ وَلَوْ كَانَ بِهِمْ خَصَاصَةٌ
“Bali wanawapendelea kuliko nafsi zao, ingawa wao wenyewe ni wahitaji.”
Hashr – 9

Abu Huraira (Radhiya Llahu anhu) amesimulia kuwa; mgeni mmoja aliyetoka safari ya mbali alimwendea Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) na kumwambia:
“Mimi nimechoka sana”.
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) (alitaka kumkirimu yeye mwenyewe, lakini) hakuwa na chochote nyumbani kwake cha kuweza kumkirimu mgeni yule. Akawauliza Sahaba zake (Radhiya Llahu anhum):
“Nani atakayemkirimu mgeni huyu usiku wa leo?”
Mmoja katika watu wa Madina akasema:
“Mimi, ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu”.
Akamchukua na kwenda naye mpaka nyumbani kwake na kumwambia mkewe:
“Tumkirimu, huyu ni mgeni wa Mtume wa Mwenyezi Mungu”.
Katika riwaya nyingine, imepokelewa kuwa alisema kumuuliza mkewe:
“Kuna chakula chochote nyumbani?”
Mkewe akajibu:
“Hakuna chochote isipokuwa chakula cha watoto wetu tu”.
Akasema:
“Wababaishe kwa chochote kile, na njaa itakapowashika sana wakataka kula chakula chao cha usiku, jaribu kuwalaza, watakapoingia wageni wetu nyumbani, zima taa, kisha tujifanye kama na sisi tunakula nao.”
Wakawakaribisha, wageni wakala, na wao wakalala na njaa yao.
Asubuhi yake alipokwenda kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam), Mtume akamwambia:
“Mwenyezi Mungu amefurahishwa na yale mliyowatendea wageni wenu usiku wa jana”.
Bukhari na Muslim

Tabia njema zilioje na nafsi njema zilioje, kwa hakika watu hawa walikuwa na ukarimu usio na kifani.

Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) aliwapa sifa za aina ya pekee watu wa kabila la Al Ash'ariy, na hili ni kabila la Sahaba maarufu Abi Musa Al Ash ary (Radhiya Llahu anhu).
Akasema:
“Watu wa kabila la Al Ash'ary wanapokuwa safarini sehemu za mbali kwa ajili ya kupigana Jihadi, watu wao walioko Madina chakula cha watoto kikipungua, basi hukusanya kile walichonacho katika kitambaa kimoja, kisha wakagawana sawa sawa baina yao. Kwa hivyo wao ni wenzangu na mimi mwenziwao”.
Bukhari na Muslim
Atakayesoma juu ya mwenendo wa Waislam na kudurusu sira zao, akaona namna gani walivyokuwa wakikirimiana, atatambua maana ya kauli yake Subhanahu wa taala ِAliposema:
وَالَّذِينَ تَبَوَّؤُوا الدَّارَ وَالايمَانَ مِن قَبْلِهِمْ يُحِبُّونَ مَنْ هَاجَرَ إِلَيْهِمْ ولا يَجِدُونَ فِي صُدُورِهِمْ حَاجَةً مِّمَّا أُوتُوا وَيُؤْثِرُونَ عَلَى أَنفُسِهِمْ وَلَوْ كَانَ بِهِمْ خَصَاصَةٌ وَمَن يُوقَ شُحَّ نَفْسِهِ فَأُوْلَئِكَ هُمُ الْمُفْلِحُونَ
“Na walio na maskani zao na Imani yao kabla yao, wanawapenda walio hamia kwao, wala hawaoni choyo katika vifua vyao kwa walivyo pewa (Wahajiri), bali wanawapendelea kuliko nafsi zao, ingawa wao wenyewe ni wahitaji. Na mwenye kuepushwa uchoyo wa nafsi yake, basi hao ndio wenye kufanikiwa."
H’ashr – 9
Likiwepo kundi la watu wasiokuwa na mwamana wala ahadi, basi watu wa aina hii hawawezi hata kidogo kuaminiana wenyewe kwa wenyewe, na hali zao zinakuwa mfano wa wanyama. Hawajali kitu isipokuwa kupata wanachokitaka hata kama kupata kwao huko kutasababisha maafa kwa wenzao.
Kwa ajili hiyo Mwenyezi Mungu ametuteremshia aya nyingi zinazotuhimiza juu ya kuwajibika kurudisha amana za watu na kutimiza ahadi.
Mwenyezi Mungu ِAnasema:
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُواْ لاَ تَخُونُواْ اللّهَ وَالرَّسُولَ وَتَخُونُواْ أَمَانَاتِكُمْ وَأَنتُمْ تَعْلَمُونَ
“Enyi mlio amini! Msimfanyie khiana Mwenyezi Mungu na Mtume, wala msikhini amana zenu, nanyi mnajua.”
Al Anfal – 27

Na Akasema:
إِنَّ اللّهَ يَأْمُرُكُمْ أَن تُؤدُّواْ الأَمَانَاتِ إِلَى أَهْلِهَا
“Hakika Mwenyezi Mungu anakuamrisheni mzirudishe amana kwa wenyewe”.
An Nisaa – 58

Na Anasema:
وَأَوْفُواْ بِالْعَهْدِ إِنَّ الْعَهْدَ كَانَ مَسْؤُولاً
“Na timizeni ahadi. Kwa hakika ahadi itasailiwa.”
Al Israa (Bani Israil) – 34

Na Akasema:
وَأَوْفُواْ بِعَهْدِ اللّهِ إِذَا عَاهَدتُّمْ
“Na timizeni ahadi ya Mwenyezi Mungu mnapo ahidi”.
An Nahl – 91

Na Akasema:
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُواْ أَوْفُواْ بِالْعُقُودِ
“Enyi mlio amini! Timizeni ahadi.”
Al Maidah – 1
Na Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) kaviingiza vitendo vya kusema uwongo, kuvunja ahadi na kuikhini amana katika dalili za Unafiki.
Katika hadithi iliyosimuliwa na Abu Huraira, Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amesema:
“Alama za mnafiki ni tatu; Akizungumza husema uwongo, akiahidi hatimizi na akiaminiwa hufanya khiana.”
Bukhari na Muslim

Na kutoka kwa Abdillahi bin Amru bin Al Aas; kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amesema:
“Tabia nne, yeyote aliyekuwa nazo (tabia hizi) anakuwa mnafiki halisi. Na aliyekuwa na moja kati ya tabia hizo, amekuwa na moja wapo ya tabia za unafiki mpaka aiache (tabia hiyo); Anapoaminiwa hufanya hiana, anapozungumza husema uwongo, anapoahidi huenda kinyume, na anapochukizwa huvuka mipaka (katika ghadhabu).”
Bukhari na Muslim
Mwenyezi Mungu amewasifia wenye kujiepusha na ubakhili.
Mwenyezi Mungu Anasema:
وَمَن يُوقَ شُحَّ نَفْسِهِ فَأُوْلَئِكَ هُمُ الْمُفْلِحُونَ
“Na wenye kuepushwa na ubakhili wa nafsi zao, hao ndio wenye kufaulu.”
At Taghabun – 16

Na wale waliojidanganya nafsi zao kwa kuona kuwa katika ubakhili mna kheri, Mwenyezi Mungu anawaonya juu ya adhabu kali inayowangojea.
Mwenyezi Mungu ِAnasema:
وَلاَ يَحْسَبَنَّ الَّذِينَ يَبْخَلُونَ بِمَا آتَاهُمُ اللّهُ مِن فَضْلِهِ هُوَ خَيْرًا لَّهُمْ بَلْ هُوَ شَرٌّ لَّهُمْ سَيُطَوَّقُونَ مَا بَخِلُواْ بِهِ يَوْمَ الْقِيَامَةِ وَلِلّهِ مِيرَاثُ السَّمَاوَاتِ وَالأَرْضِ وَاللّهُ بِمَا تَعْمَلُونَ خَبِيرٌ
“Wala wasione wale ambao wanafanya ubakhili katika yale aliyowapa Mwenyezi Mungu katika fadhila Zake kuwa ni bora kwao (kufanya ubakhili huko). La!, ni vibaya kwao. Watafungwa kongwa (madude ya kunasa shingoni) za yale waliyoyafanyia ubakhili – Siku ya Kiama”.
Aali Imran – 180

Na ِAkasema:
وَالَّذِينَ يَكْنِزُونَ الذَّهَبَ وَالْفِضَّةَ وَلاَ يُنفِقُونَهَا فِي سَبِيلِ اللّهِ فَبَشِّرْهُم بِعَذَابٍ أَلِيمٍ. يَوْمَ يُحْمَى عَلَيْهَا فِي نَارِ جَهَنَّمَ فَتُكْوَى بِهَا جِبَاهُهُمْ وَجُنوبُهُمْ وَظُهُورُهُمْ هَـذَا مَا كَنَزْتُمْ لأَنفُسِكُمْ فَذُوقُواْ مَا كُنتُمْ تَكْنِزُونَ
“Na wanao kusanya dhahabu na fedha, wala hawazitumii katika Njia ya Mwenyezi Mungu, wabashirie khabari ya adhabu iliyo chungu.
Siku zitapo tiwa moto katika Moto wa Jahannamu, na kwazo vikachomwa vipaji vya nyuso zao na mbavu zao na migongo yao, wakaambiwa: Haya ndiyo mlio jilimbikia nafsi zenu, basi onjeni mliyo kuwa mkilimbika.”
At Tawba – 34 – 35

Na ubakhili unaangamiza jamii, kwani kwa ajili yake (ubakhili), damu nyingi zilimwagika, na heshima zilivunjwa.
Imepokelewa kutoka kwa Imam Muslim kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amesema:
“Uogopeni ‘Jiepusheni’ na ubakhili, kwa sababu ubakhili uliwaangamiza wale waliokuwepo kabla yenu, uliwafanya wamwage damu zao na wakubali heshima za wanawake zao zivunjike”.
Kwa kawaida mwanadamu huipenda sana mali yake. Kwa ajili hiyo Mwenyezi Mungu ametuletea aya nyingi zikituelezea juu ya thawabu pamoja na ujira mkubwa watakaoupata wale watakaozitoa mali zao katika njia anazozipenda Mwenyezi Mungu na kuridhika nazo.
Mwenyezi Mungu Anasema:
مَّن ذَا الَّذِي يُقْرِضُ اللّهَ قَرْضًا حَسَنًا فَيُضَاعِفَهُ لَهُ أَضْعَافًا كَثِيرَةً وَاللّهُ يَقْبِضُ وَيَبْسُطُ وَإِلَيْهِ تُرْجَعُونَ
“Ni nani atakeyemkatia Mwenyezi Mungu sehemu bora (ya mali yake kwa kuwapa masikini na kutoa katika mambo mengine ya kheri) ili Mwenyezi Mungu amzidishie mzidisho mwingi na Mwenyezi Mungu ndiye anayezuwia na ndiye anayetowa na Kwake (nyote) mtarejeshwa.”
Al Baqarah – 245

Na Akasema:
وَسَارِعُواْ إِلَى مَغْفِرَةٍ مِّن رَّبِّكُمْ وَجَنَّةٍ عَرْضُهَا السَّمَاوَاتُ وَالأَرْضُ أُعِدَّتْ لِلْمُتَّقِينَ. الَّذِينَ يُنفِقُونَ فِي السَّرَّاء وَالضَّرَّاء وَالْكَاظِمِينَ الْغَيْظَ وَالْعَافِينَ عَنِ النَّاسِ وَاللّهُ يُحِبُّ الْمُحْسِنِينَ
“Na yakimbilieni maghfira ya Mola wenu Mlezi, na Pepo ambayo upana wake ni sawa na mbingu na ardhi, iliyo wekwa tayari kwa wachamngu.
Ambao hutoa wanapo kuwa na wasaa na wanapo kuwa na dhiki, na wanajizuia
ghadhabu, na wasamehevu kwa watu; na Mwenyezi Mungu huwapenda wafanyao wema.”
Aali Imran – 133 – 134

Na Akasema:
فَأَمَّا مَن أَعْطَى وَاتَّقَى. وَصَدَّقَ بِالْحُسْنَى. فَسَنُيَسِّرُهُ لِلْيُسْرَى
“Ama mwenye kutoa na akamcha Mungu. Na akaliwafiki lilio jema. Tutamsahilishia yawe mepesi.”
Al Layl – 5 – 7
Mtu hasidi ni mtu mouvu sana anayeudhika na kuumia moyoni pake kila wenzake wanapofurahi na kila wenzake wanapopata mafanikio au wanaponeemeka. Kila anapomuona mtu amepata neema, basi hutamani neema hiyo imuondokee na imjie yeye. Na huenda hata akajitahidi katika kufanya baadhi ya vitimbi ili aipate yeye neema hiyo.
Mtu hasidi si rahisi kupona kutokana na maradhi yake hayo, ndiyo sababu Mwenyezi Mungu akatutaka tujikinge Kwake kutokana na shari ya hasidi anapohusudu.
Mwenyezi Mungu ِAnasema:
قُلْ أَعُوذُ بِرَبِّ الْفَلَقِ 1 مِن شَرِّ مَا خَلَقَ 2 وَمِن شَرِّ غَاسِقٍ إِذَا وَقَبَ 3 وَمِن شَرِّ النَّفَّاثَاتِ فِي الْعُقَدِ 4 وَمِن شَرِّ حَاسِدٍ إِذَا حَسَدَ 5
1.   “Sema: Najikinga kwa Mola Mlezi wa mapambazuko,
2.   Na shari ya alivyo viumba,
3.   Na shari ya giza la usiku liingiapo,
4.   Na shari ya wanao pulizia mafundoni,
5.   Na shari ya hasidi anapo husudu.”
Al Falaq

Uhasidi ni dhambi ya mwanzo aliyoasiwa Mwenyezi Mungu, kwa sababu kilichomfanya Ibilisi akatae kumsujudia Adam ni husda. aliposema:
قَالَ أَنَاْ خَيْرٌ مِّنْهُ خَلَقْتَنِي مِن نَّارٍ وَخَلَقْتَهُ مِن طِينٍ
“Mimi ni bora kuliko yeye. Umeniumba kwa moto, naye umemuumba kwa udongo.“
Al Aaraf – 12

Mayahudi nao walimkanusha Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) kwa sababu ya uhasidi wao. Kisha hawakutoshelezwa na hayo, wakafanya kila aina ya vitimbi wapate kuwatoa Waislam katika dini yao.
Mwenyezi Mungu Anasema:
وَدَّ كَثِيرٌ مِّنْ أَهْلِ الْكِتَابِ لَوْ يَرُدُّونَكُم مِّن بَعْدِ إِيمَانِكُمْ كُفَّاراً حَسَدًا مِّنْ عِندِ أَنفُسِهِم
“Wengi miongoni mwa watu wa Kitabu wanatamani lau wange kurudisheni nyinyi muwe makafiri baada ya kuamini kwenu, kwa ajili ya uhasidi uliomo ndani ya nafsi zao.”
Al Baqarah – 109

Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) ameutahadharisha Umma wake juu ya kitakacho sababisha kufarikiana wao kwa wao na kujenga chuki baina yao. Yaliyo msitari wa mbele kabisa katika yanayosababisha hayo ni husda.
Katika Sahih Muslim, kutoka kwa Abu Huraira (Radhiya Llahu anhu) kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amesema:
“Msioneane husda wala msifanyiane hiana, wala msichukiane, wala msiendeane kinyume, wala mtu asiuze kile alichokwisha muuzia mwenzake na kuweni (enyi) waja wa Mwenyezi Mungu ndugu”.
Si katika uhasidi mtu kutamani kupata neema aliyopata mwenzake kwa nia nzuri, bali huko kunaitwa ‘kutamani’, tofauti na kuhusudu.
Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu alayhi wa sallam) amesema:
“Hairuhusiwi husuda isipokuwa katika mambo mawili;
Mtu, Mwenyezi Mungu amempa mali, akawa anaitowa katika njia ya Mwenyezi Mungu usiku na mchana, na mtu Mwenyezi Mungu amempa Qurani, (amehifadhi vizuri Qurani), anaamka usiku na kuswali pamoja na mchana huku akiisoma.”

Mwanadamu akizichunguza neema za Mola wake alizomneemesha nazo, kisha akamtizama yule aliye duni yake akihangaika na dunia, lazima itamuondoka husda aliyo nayo na ataanza kushukuru.
Wasalaamun ala l Mursaliyna wa l hamdu li Llahi rabbi l aalamiyn