Sunday, December 1, 2013

kikao cha wanajumuiya  wa msateku kilichofanyika December mosi 2013 katika msikiti wa JIDDAH .. kama wanavyoonekana katika picha..

Baadhi ya Ma-Ukhuti walioudhuria katika kikao icho.....

        hawa ni baadhi ya viongozi walioendesha kikao... wakiwa na Amir wa JUMUIYA al-akhy Abdul.


Wednesday, October 30, 2013

kikao cha wanajumuiya wa MSATEKU kilichofanyika oktoba 27 katika msikiti wa wanajumuiya wa msateku... katika kikao icho waliudhulia baadhi ya waitimu wa 2010/13 ambao walikuwa wanajumuiya...miongoni mwao alikuwepo akhy SESEME, brother JARIBU na RIZIWANI..

  baadhi ya matukio...... wakati wa kikao......


Baada ya kikao wanajumuiya walikwenda JIDDAH RESTAURANT kupata chakula cha mchana.. 
karibuni sana JIDDAH kunachakula kizuri na tunawapishi mahili kabisa... bila shaka ukifika JIDDAH RESTAURANT roho yako itasuuzika kwa uduma zetu...

Saturday, October 26, 2013

Mahafali ya TEKU 2013

Siku ya tarehe 26/10/2013.....chuo cha TEKU kiliazimisha mahafali ya Sita(6) tangu kuanzishwa kwake....baadhi ya Wanajumuiya na viongozi wa wastaafu wa Msateku walikuwa washiriki wa mahafali hiyo.....lakini cha kumshukuru ALLAH kiongozi mstaafu wa Idara ya Elimu katika MSATEKU pia alikuwa Naibu Amir wa TAMSYA Mbeya AMOUR ABDALLAH....alitunukiwa zawadi ijulikanayo kama TEKU PRIZE baada ya kufanya vizuri katika masomo kwa mwaka 2010-2013 kwa kupata matokeo ya jumla ya G.P.A ya 4.7 hakika anapaswa kupongezwa na pia Jumuiya ya MSATEKU....zifuatazo ni baadhi ya matukio hayo.


Mshindi wa zawadi ya TEKU PRIZE....Amour Abdallah....aliibuka kidedea kama mwanafunzi bora katika mwaka wa masomo 2010-2013 kwa kupata G.P.A ya 4.7......HONGERA SANA BROTHER.....!!!!

 Baadhi ya viongozi wastaafu waliohitimu 2013 kutoka kulia ni Brother Jaribu,Kato Mudathiru,Hassan Mavue na Seseme Shaabani.

 Hakika ni kwa kumshukuru Mungu.....BROTHER JARIBU (katibu mkuu Mstaafu wa MSATEKU) nae alikuwepo....hapo ni katika maandamano.
 kabla ya mahafali kuanza......
 hakika ilifana.....
 zawadi zilitolewa......
 Tabasamu baada ya kumaliza DEGREE ya kwanza....HONGERENI SANA.

TAKBIRR......!!!!!!TAKBIRRR.........!!!!TAKBIRRR......!!!!

Assalam Alaykum.....!!!!!wanajumuiya wa MSATEKU na wale waislamu wote kwa ujumla ......hatuna budi kumshukuru ALLAH.....kwa hatua tuliyofikia hivi sasa katika maendeleo ya MRADI wetu wa Mgahawa....hakika ALLAH wa kushukuliwa katika yote mazuri tuliyoyafikia......Tayari mradi wetu wa Mgahawa umeanza kazi na mambo yanaendelea ndani ya MSATEKU.....Mgahawa unaitwa JIDDAH....na umeanza kuwa maarufu katika eneo la BLOCK T.......zifuatazo ni picha za Mgahawa huo...ndani na nje.....yapata mwezi sasa tangu kuanza rasmi.....ulianza tarehe 26 /09/ 2013.
 Jiddah Restaurant.....ndio maneno yanayosemeka kwa nje ya mgahawa wetu

 Ndani ya mgahawa kuna wateja na wafanyakazi wetu.....suala la usafi na muonekano nadhifu limezingatiwa.
 karibu mteja...........
 mambo ya asubuhi hayoo....chai ya maziwa, ya Mdarasini....,Tangawizi......pamoja na SUPU ya Ngo'mbe utapata.

 Hakika kunavutia........karibuni sanaaa JIDDAH.....



Wednesday, July 10, 2013

Mawaidha kwa njia ya Video Mada watu Kumi waliosamehewa kufunga na Shekh Nurdin Kishk........!!!!!!!karibuni sana....


Msateku wafuturu kwa pamoja........

As.alaykum....!!!!huku mitihani ikiendelea ambapo hatimaye ni Kesho sawa na tarehe 11/7/2013, Msateku kwa pamoja leo walipata futari ya pamoja katika chungu Mosi...hakika ilivutia na ilikuwa rahaa kwa vijana hawa.....nakupatia baadhi ya picha za tukio hilo...lilofanyika katika Mgahawa na Msikiti wa Jumuiya.

 baadhi ya wanajumiuya pichani...wakipata futariii
 Maukht nao walikuwepo.......wakipata futuruuuuuuuuuu

Mwalimu Rais Mwinyi katika Tamasha la Kiswahili









Rais Mstaafu, Mwalimu A. H. Mwinyi akihutubia katika maadhimisho ya Tamasha la Kiswahili.
Rais Mstaafu, Mwalimu Ali Hassan Mwinyi siku ya Jumamosi Juai 6, 2013 katika ukumbi wa Hamton Place alikamilisha sherehe za miaka 3 ya blog ya Vijimambo pamoja na Tamasha la Kiswahili lililoandaliwa na Jumuiya ya Watanzania na uongozi wa Ubalozi wa Tanzania Jijini Washington DC, nchini Marekani.

Baadhi ya Watanzania kutoka maeneo mbalimbali walihudhuria na kuisikiliza hotuba ya Rais na Mwalimu Mwinyi aliyoitoa ambayo iligusia misingi ya matumizi ya baadhi ya maneo ya Kiswahili ambayo tunayatumia kwa makosa kwa kuchanganya umoja ama wingi wake. Alitoa mifano ya matumizi ya maneno yafutayo:

UMOJA na WINGI

Ni sahihi kusema “madhehebu” na siyo sahihi kusema, “dhehebu”. Neno madhehebu halina wingi. Hakuna neno dhehebu.

Ni sahihi kusema mahitaji, lakini si sahihi kusema hitaji

Mafao
 na siyo fao

Ni mahakama, hakuna hakama
Majuto ni neno moja, hakuna neno juto

Mateso
 ni sahihi, hakuna teso

Sahihi kusema madhila na siyo dhila

Maradhi
 na siyo radhi (radhi ni neno jingine lenye maana nyingine. Mathalani kumwona mwendawazimu na 
kusema, "yule kakosa radhi kwa baba yake...")

Neno shule halina wingi (ni singular, asili yake Kijerumani), Shule moja, shule hamsini (hakuna mashule)

Askari (akiwa mmoja, wakiwa mia bado ni askari) siyo maaskari

Polisi (mmoja au wengi) hakuna neno mapolisi

Saa (saa haina wingi). Si sahihi kusema, “nimesafiri kwa masaa mengi” bali sahihi kusema nimesafiri kwa saa...)

Hesabu (haina wingi, inabakia kuwa hesabu) hakuna mahesabu

Upungufu, hakuna neno mapungufu

Uamuzi
, hakuna neno maamuzi

Ni uhusiano, hakuna neno mahusiano

Na ni ushirikiano, siyo neno mashirikiano. Halipo neno hilo katika Kiswahili sanifu.


MATUMIZI YA SILABI

Matumizi ya silabi 'sha' maana yake ni kisababishi/inasababisha. Kwa mfano, si sahihi kusema, "Nimemwenda Marekani sina nyumba ilinibidi nikodishe" kwa kuwa kama huna kitu, wewe utasema, "Nimekwenda Marekani sina nyumba ilinibidi nikodi". Mimi sina nyumba nikodishe? Na mwenye nyumba akodishe? Hapana, 'sha' ni kisababishi. Asiye na nyumba akodi, na mwenye nyumba akitaka akodisha. Ama, “Juma nusura kunifukuzisha kazi kwa fitina yake”. Yaani ningefukuzwa kazi kwa fitina ya Juma.

KUHESABU

Hesabu: Vitu huhesabiwa moja, mbili, tatu n.k., ila watu huhesabiwa mmoja, wawili, watatu, wanane, tisa n.k., kwa sababu maneno tunayoyaazima kutoka kwenye lugha nyinginezo, tusiyaingilie kuyachokoa. Sita, Saba, Tisa ni Kiarabu, si Kiswahili, ndiyo maana twasema Watu, ng’ombe sita, saba, tisa.